KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, January 11, 2014

Moyes akanusha kupoteza 'network' na wachezaji wake

David Moyes amekanusha kwamba uhusiano wake na nyota wa kikosi chake umezorota akisema kuwa wachezaji wake wanamuunga mkono, huku shinikizo dhidi ya meneja huyo wa magwiji, Manchester United, likiendelea.

Moyes amekumbwa na mashaka tangu kuchukua kazi ya kukiongoza kikosi cha mabingwa hao wa Ligi ya Premier ya Uingereza Julai na mwaka mpya umemwongezea majonzi.

United wamepoteza mechi tatu mtawalia za kufungua mwaka kwa mara ya kwanza tangu 1932 huku Tottenham, Swansea katika kombe la FA na Sunderland katika lile la League Cup wakiwatepetesha kabisa. 

Licha ya hayo, Moyes ameshikilia kwa dhati kwamba hajapoteza utawala wa wachezaji wake ambao hawana uzoefu wa kuchakazwa kila kuchao.
“Sidhani wachezaji wamejificha,” meneja huyo ambaye klabu chake kina mwanya wa pointi 11 nyuma ya viongozi wa Premier, Arsenal, alisema.
“Kila mmoja wao amesimama kidete na kufanya kila liwezekanalo. Hauwezi kuamrisha yeyote atie bidii zaidi ya uwezo wake na vijana wangu wamekuwa wakifanya hivyo,” aliongeza.
Huku Arsenal wakisubiri hadi Jumatatu kucheza kwenye ligi watakapo watembelea Aston Villa, Chelsea, wanaoketi nafasi ya tatu wana nafasi ya kumiliki uongozi ikiwa watatamba ugenini Hull City Jumamosi.

No comments:

Post a Comment