KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, July 5, 2014

E.Guinea nje ya CAN 2015.

Equatorial Guineanje ya michuano ya Afrika
Equatorial Guinea imeondolewa nje ya mashindano ya kuwania tikiti ya kuwania ubingwa wa Afrika mwakani huko Morocco.

Kamati inayosimamia michuano hiyo  imeipata taifa hilo na hatia ya kumchezesha mchezaji kinyume na kanuni za shirikisho la soka duniani FIFA.

Kamati hiyo simamizi iliipata E. Guinea na hatia ya kumshirikisha mzaliwa wa Cameroon Thierry Fidieu Tazemeta, katika ushindi wao wa mkondo wa kwanza dhidi ya Mauritania tarehe 17 Mei.

Hakuna ushahidi uliotolewa kudhibitisha kuwa Tazemeta alikuwa kabadili Uraia .

Mauritania ilikuwa imeuliza kudhibitishwa kwa uraia wa mchezaji huyo katika mkondo wa kwanza ilipoibuka mshindi wa 1-0.

Equatorial Guinea hata hivyo ilipuuza madai hayo na ikamshirikisha katika mechi ya pili ambayo E .Guinea iliibuka na ushindi mkubwa wa 3-0 .

Kufuatia kauli hiyo Mauritania imerejeshwa mashindanoni na sasa itakabiliana na Uganda katika mkondo wa mwisho wa kufuzu.

Mwaka uliopita Equatorial Guinea ilipoteza mechi mbili kwa sababu sawa na hizo katika mechi ya kufuzu kwa dimba la dunia la Brazil,2014.

No comments:

Post a Comment