KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 18, 2014

Kocha Joachim Löw wa Ujerumani ana saka msaidizi wake baada ya kutwaa taji la dunia nchini Brazil

Licha ya mafanikio ya kutwaa taji la kombe la dunia kwenye ardhi ya taifa lenye wendawazimu mkubwa wa soka dunia Brazil, Joachim Löw ameyaangazia macho yake kwa changamoto zijazo kwa lengo la kufika mbali zaidi kimafanikio kama ilivyokuwa kwa Uhispania kama Mabingwa wa Ulimwengu na Ulaya.
Kwasasa kocha huyo wa Ujerumani yuko mawindoni kumtafuta msaidizi wake mpya. 
Naibu kocha Hans-Dieter Flick, amekuwa msaidizi wa Löw tangu mwaka wa 2006, wakati Löw alipoichukua mikoba kutoka kwa Jürgen Klinsmann baada ya kukamilika Kombe la Dunia lililoandaliwa katika ardhi ya nyumbani.
 Kuanzia Septemba mosi, Flick atachukua kazi ya mkurugenzi mkuu wa Shirikisho la Soka Ujerumani - DFB.
Mwezi wa Septemba utakuwa wenye shughuli nyingi kwa Die Mannschaft.
 Pembeni ya uteuzi huu, pia kutakuweko na mechi za kirafiki dhidi ya Argentina walioshindwa katika fainali, na Scotland.
Mnamo Oktoba 2013, Löw aliurefusha mkataba wake na Shirikisho la DFB hadi mwishoni mwa mashindano ya UEFA Euro 2016. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 53 kisha atakuwa amekamilisha kipindi cha mwongo mmoja kama kocha wa Ujerumani.
Kocha wa zamani wa Mainz Thomas Tuchel anaripotiwa kuwa mmoja wa majina yanayotarajiwa kujaza pengo la naibu kocha wa taifa. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 39 alihama klabu ya Mainz kwa ghafla mwishoni mwa msimu uliopita wa Bundesliga licha ya kuisaidia klabu hiyo kufuzu katika dimba la Europa League kwa mara ya pili katika historia ya klabu hiyo.
Rais wa DFB Niersbach ameweka wazi kuwa Löw atafanya uamuzi kamili kuhusiana na nafasi hiyo, na hapatakuwa na hali yoyote ya kuingilia kati kwa maafisa wengine wa DFB pamoja na wadau wa soka Ujerumani.

No comments:

Post a Comment