KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 8, 2014

Mashabiki wa Colombia watangaza uadui na beki aliyemjeruhi Neymar, Juan Zuniga,

Sehemu ya mashabiki wa Colombia wakati wa kuipokea timu yao ikirejea kutoka Brazil
Timu ya taifa ya Colombia iliondolewa kwenye fainali za kombe la dunia katika hatua ya robo fainali baada ya kufungwa mabao mawili kwa moja dhidi ya wenyeji timu ya taifa ya Brazil.

Mashabiki wa soka nchini Brazil wametangaza uadui wa maisha na beki wa pembeni wa tyimu ya taifa ya Colombia Juan Zuniga, baada ya kuchuikizwa na rafu aliyomfantyia mshambuliaji wake Neymar Da Silva Junior.

Mashabiki wa soka nchini Brazil wamethibitisha kwa vitendo vita yao dhidi ya beki huyoa mbae anaitumikia klabu ya Societa Sportiva Calcio Napoli ya nchini Italia kwa kuchana hadharani karata zenye picha yake.

 Mashabiki hao wamesema katu hawawezi kumsamehe Zuniga, kutokana na kosa alilowafanyia la kumuumiza muokozi wao ambapo aliamini angefanikisha kila jambo walilolikusudia.

Hata hivuyo mashabiki hao wamelitaka shirikisho al soka duniani FIFA kutoa adhabu kali kwa Juan Zuniga, kutokana na kuamini kwamba limcheza rafu kwa makusudi dhidi ya Neymar.

Tayari imeshaelezwa kwamba Neymar hatocheza tena katika michezo ya kombela dunia iliyosalia baada ya kuonekana amepata majeraha katika sehemu ya mfupa unaoshikilia uto wa mgongo.

Neymar atuma salamu kwa wenzake waliosalia kikosini
 
Wakati huo huo Neymar amesema wachezaji wenzake bado wana nafasi kubwa ya kumsaidia kutimiza ndoto ya kutwaa Kombe la Dunia.
Neymar atuma salamu kwa wachezaji wenzake
Huku akimwaga machozi, Neymar amesema kuumia kwake hakuwezi kuwa mwisho wa ndoto zake na Brazil kutwaa Kombe la Dunia
“Nafasi ipo, ninawaamini wenzangu wanaweza kufanya jambo na kutimiza ndoto.
“Mimi nilikuwa ni sehemu ya timu, hivyo bado timu ina uwezo wa kutimiza malengo yetu.
“Nawatakia wenzangu wote kila la kheri ili wafikie ndoto zetu,” alisema.

No comments:

Post a Comment