
Akiongea na Rockersports moja kwa moja kutoka kambini Tukuyu mkoani Mbeya, Kanavaro ameweka wazi kuwa ana shauku kubwa ya kurejea katika kikosi cha Yanga ambacho mbali ya ujio wa kocha Maximo lakini pia kuna nyongeza ya wachezaji wapya akiwemo Coutinho aliyetokea nchini Brazil.
Canavarro ambae kwa sasa yupo mjini Tukuyu sanjarti ya
kikosi cha timu ya Taifa, amesema amekuwa na shauku hiyo kutokana na ujio wa
kocha Maximo ambaye amekiri anamuhusudu kutokana na falsafa za ufundishaji
wake.
Amesema anampenda sana kocha huyo kutokana na mazuri
aliyomuwachia kabla hajaachana na timu ya taifa ya Tanzania mwaka 2010, hivyo
mambo yatakuwa mazuri msimu ujao.
Anaamini kikosi cha Yanga kitatisha msimu ujao kwakuwa Maximo ni kocha mzuri.
No comments:
Post a Comment