KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 14, 2014

Tuzo ya Lionel Messi ya Golden Ball ya kombe la dunia yaendelea kupingwa

Stanley Victor "Stan" Collymore,

Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Stanley Victor "Stan" Collymore, amepinga hatua ya shirikisho la soka duniani FIFA ya kumpa tuzo ya mchezaji bora wa fainali za kombe la dunia za mwaka 2014, mshambuliaji wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Andres Messi.
Messi akiwa na tuzo yake ya mchezaji bora wa mashindano ya kombe la dunia
Collymore, amesema FIFA wamechemka katika maamuzi ya kumzawadiwa tuzo hiyo, Lionel Messi kutokana na kiwango duni alichokionyesha katika mchezo wa hatua ya fainali pamoja na michezo mingine ya michuano ya mwaka huu.

Amesema wapo wachezaji wengi ambao walionyesha uwezo mkubwa na ilidhihirika wazi huenda wangepewa tuzo hilo, lakini cha kustaajabisha FIFA kwa kushirikiana na kamati ya mashindano wamemtangaza Messi, ambaye hakuonekana kama anaitumikia vyema timu yake ya taifa kama anavyokuwa kwenye klabu yake ya Barcelona.

"Kiwango chake kilikuwa duni, sijaelewa mpaka sasa kwa nini amekua Messi isiwe mchezaji mwingine kama James Rodriguez, Alexis Sanchez pamoja na Manuel Neuer” amesema Collymore.

"Hata ingelikua kuna tuzo ya mchezaji bora wa timu ya taifa ya Argentina ingelikuwa mimi nisingempa Messi, kutokana na kiwango duni alichokionyesha” Collymore.

Wengi bado wanaamini kuwa pengine tuzo hiyo ingestahili kuchukuliwa na Toni Kroos, Philipp Lahm na Sami Khedira kutoka katika kikosi cha mabingwa huku akiongezwa Arjen RobbenNeymar na hata mshindi wa tuzo ya ufungaji bora (Golden Boot) James Rodrigues na mlinda mlango Manuel Neuer (the Golden Glove winner), Keylor Navas na Sergio Romero.

Mbali na Lionel Messi kutajwa kama mchezaji bora wa fainali za kombe la dunia za mwaka 2014, zawadi nyingine kama kipa bora imekwenda kwa mlinda mlango wa timu ya taifa ya Ujerumani Manuel Neuer, huku kiatu cha dhahabu kikichukuliwa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Colombia James Rodriguez.

Zawadi zilizotolewa kwa wachezaji na timu

Adidas Golden Ball - Mchezaji bora: Lionel Messi (Argentina)
Adidas Silver Ball - Mchezaji bora 02: Thomas Muller (Ujerumani)
Adidas Bronze Ball - Mchezaji bora 03: Arjen Robben (Uholanzi)
Adidas Golden Boot – Mfungaji Bora: James Rodriguez (Colombia)
Adidas Silver Boot – Mfungaji Bora 02: Thomas Muller (Ujerumani)
Adidas Bronze Boot – Mafungaji Bora 03: Neymar (Brazil)
Adidas Golden Glove – Kipa bora: Manuel Neuer (Ujerumani)
Hyundai Young Player Award – Mchezaji bora mwenye umri mdogo: Paul Pogba (Ufaransa)
FIFA Fair Play Award – Timu yenye nidhamu: Colombia

No comments:

Post a Comment