KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 13, 2014

PSG kuwazidi kete Manchester United kunasa saini ya Di Maria

PSG sasa wanapewa nafasi kubwa ya kumsajili Di Maria wakati ambapo Manchester United wakisua sua
Paris Saint-Germain imekuwa yenye nafasi kubwa kuliko nyingine zote ambazo zinamfukuzia winga wa Real Madrid Angel Di Maria.
Winga huyo anaonekana hana nafasi tena ndani ya viunga vya Bernabeu baada ya Real kuonekana kumtaka zaidi kiungo mchezeshaji raia wa Colombia James Rodriguez kuwa ndiye mchezaji namba moja katika mawindo yao.
Top form: Di Maria had an excellent season for Real Madrid last year, including helping to win 'la decima'
 Di Maria aliisaidia Real Madrid kushinda 'la decima'


PSG kwasasa wanaamini kuwa wako mbele zaidi katika harakati za kumsajili winga huyo mwenye umri wa miaka 26 Di Maria, ambaye mkataba wake na Madrid una muda wa miaka minne.
Di Maria anawaniwa pia na Manchester United huku Madrid wenyewe wakimthaminisha kwa karibu pauni milioni £50.
Taarifa zinasema kuwa United bado haijaweka rasmi mezani mpango wa kumnasa Di Maria ingawa kuonekana kuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment