KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 7, 2014

TFF kuendesha semina maalum kupinga kampeni dhidi ya upangaji wa matokeo

Mkurugenzi wa ufundi wa TFF Salum Madadi kuendesha semina ya kupinga rushwa katika soka
Shirikisho la soka nchini TFF linajipanga kuendesha semina maalum kwa maafisa wa klabu za ligi kuu pamoja na ligi daraja la kwanza ambayo italenga kampeni dhidi ya upangaji matokeo.

Mkurugenzi wa michezo wa shirikisho hilo Salum Madadi amesema baada ya maafisa taasisi inayoendesha kampeni dhidi ya upangaji matokeo kutoka nchini Uingereza kutoa mafunzo kwa wachezaji wa timu ya taifa ya vijana pamoja na waandishi wa habari mwishoni mwa juma lililopita, hatua inayofuata itawahusu viongozi wa klabu za ligi kuu na daraja la kwanza.

Madadi amesema lengo kubwa la kuwahusisha viongozi wa klabu za ligi kuu na daraja la kwanza ni kutaka kutoa elimua mbayo itakuwa tahadhari kwa viongozi hao ambao kwa asilimia kubwa huenda wakawa chanzo cha kujihusisha suala la upangaji wa matokeo.
Hata hivyo Salum Madadi amesema kamepeni dhidi ya upangaji wa matokeo haitoishia kwa viongozi wa klabu za ligi kuu pamoja na daraja la kwanza, bali wataifikisha hadi kwa vijana wanaochipukia kwenye medani wa soka.

No comments:

Post a Comment