Nani alionywa na mwamuzi Nuno Almeida wakati wa mchezo dhidi ya Arouca |
Kukosa penati kwa winga wa Manchester United Luis Nani aliyeko kwa mkopo katika klabu ya Sporting Lisbon imekuwa ni swali kubwa juu ya uwezo wake, na kitendo cha kubadilishwa katika dakika ya 77 katika mechi yake ya kwanza katika klabu ya Sporting Lisbon inakuwa ni majibu ya kwanini mashabiki wa soka wa Manchester United kwanini hawajutii kumkosa winga huyo.
Nani, ambaye alijiunga na klabu yake ya zamani kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu mpya 2014/2015 anaonekana hakuwa na faida kwa United ambapo dili la kusajiliwa Marcos Rojo linaonekana limefanyika kwa wakati muafaka.
Winga huyo wa kimataifa wa Ureno alipata nafasi ya kufunga katika mchezo wake wa kwanza akiwa Sporting Lisbon kunako dakika 63 lakini alishindwa kufanya hivyo katika eneo la miguu 12 dhidi ya timu ya Arouca.
Nani alitegemewa kuonyesha kiwango katika mchezo wa kwanza akiwa na klabu yake ya zamani ya Sporting Lisbon
Penati ya Nani yapanguliwa na mlinda mlango wa Arouca Mauro Goicoechea
Karibu nyumbani: Nani akishangiliwa na mshabiki wa Sporting Lisbon muda mfupi baada ya kutua Ureno
Katika mchezo huo Sporting ilisawazisha goli katika dakika ya mwisho kupitia kwa Carlos Mane ambapo wengi wanadhani kuwa hiyo inaweza kuibua presha mpya kwa Nani.
Nani,ambaye aliingia mkataba wa miaka mitano na Manchester United mwezi Septemba, ameshindwa kumshawishi Louis van Gaal katika kikosi chake cha kwanza.
Kumbuka, Rojo amepishana na Nani lakini hataweza kuanza katika kikosi cha Manchester United dhidi ya Sunderland Jumapili kwakuwa klabu yake bado haijapokea kibali kwa wakati mchezo utakapigwa Stadium of Light.
Rojo akiwa na Van Gaal |
No comments:
Post a Comment