Luis Suarez akipiga picha na nahodha wake wa zamani Steven Gerrard (akionyesha jezi ya Barcelona ambayo ilikuwa ni zawadi kwa Gerard) katika uwanja wa mazoezi wa Melwood hii leo Jumatatu |
Luis Suarez amerudi kwa mara nyingine tena katika uwanja wa Liverpool siku ya mwisho ya kufungwa kwa dirisha la usajili lakini kubwa ni kwamba mshambguliaji huyo aliyenunuliwa kwa pauni milioni £75 na Barcelona alikuwenda kusafisha sanduku lake na kuondoka na kila kilichokuwa chake.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alielekea huko akiwa na zawadi ya jezi ya Barcelona kwa Steven Gerrard ambapo alipiga picha akiwa na nahodha wake huyo wa zamani wakiwa wameshikilia zawadi hiyo na kuitupia katika ukurasa wake wa Instagram.
Kwaherini: Suarez akiwa wachezaji wenzake wa zamani Gerrard (kushoto), Glen Johnson (wa pili kulia) na Jon Flanagan
Tunafunga dirisha: Suarez akiondoka katika viunga vya Melwood hii ikiwa ni siku ya mwisho ya kufungwa kwa dirisha la usajili akiwa na sanamu la mtoto katika kiti cha nyuma
No comments:
Post a Comment