KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 15, 2014

Huyu ni Lucas Silva wa Cruziero ya Brazil ambaye endapo atasajiliwa tu na Madrid basi Sami Khedira ni mali ya Arsenal kila kitu kipo kwenye mstari


Baada ya Arsenal kupiga hatua moja mbele na kukaribia kukamilisha usajili wa kiungo Sami Khedira baada ya Real Madrid kukubali kufungua mazungumzo ya kusajili mbadala wake.

Washika mitutu wanadhaniwa wamekubali kimsingi juu ya vipengele vinavyomuhusu mchezaji mwenyewe kwa maana ya Khedira ikiwa kusafisha barabara ya kujiunga na Emirates Stadium, ambapo sasa ada ya uhamisho ikiwa ndio mjadala ulioko mezani ukijadiliwa na pande mbilo hizi.

Na kinachoonekana ni kama kumalizia taratibu tu yaani kufuata njia ya halali ambapo gazeti la Marca limeripoti kuwa Arsenal watakuwa huru kumchukua Khedira endapo Madrid watafanikiwa kumnasa nyota wa Cruziero Lucas Silva.
Huyu ni Lucas Silva wa Cruziero ya Brazil ambaye endapo atasajiliwa tu na Madrid basi Sami Khedira ni mali ya  Arsenal
Madrid wameanza mazungumzo juu ya namna ya kumpata Silva na wamamatumaini kuwa kiasi cha pauni milioni £15 walichotenga kwa ajili ya Silva kitakubaliwa na kwamba hiyo ni fursa kwa Khedira kujiunga na Arsenal.

No comments:

Post a Comment