KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 15, 2014

Mesut Ozil ndani ya tuhuma nzito za mapenzi akimsaliti mpenzi wake mwanamuziki Capristo

Ozil na mpenzi wake Capristo wakiondoka katika mgahawa wa Zuma jijini London Oktoba 2013
Nyota wa Arsenal Mesut Ozil ameanikwa mbele ya umma na mchezaji mwenzake wa Ujerumani kuwa amekuwa akimsaliti kimapenzi mpenzi wake nyota wa muziki wa Pop Mandy Capristo.

Mchezaji wa zamani wa Bayern Munich na Hertha Berlin Christian Lell amemtuhumu Ozil kuwa amekuwa akimtunishia misuli juu ya mahusiano yake na mpenzi wake wa zamani Melanie Rickinger.

Katika mahojiano na Bild, Lell bila ya aibu amemuelezea mpenzi wake huyo wa zamani kuwa ni kama nyoka na kueleza kuwa amekuwa akibadilishana jumbe za mapenzi na Ozil kupitia huduma ya ujumbe mfupi ya WhatsApp.
Mesut Ozil has been accused of cheating on girlfriend Mandy Capristo by ex-Bayern player Christian Lell
Mesut Ozil ameshutumiwa kwa kumsaliti wa kimapenzi kwa mpenzi wake Mandy Capristo kwa kuwasiliana kwa jumbe za mapenzi na mpenzi wa zamani wa nyota wa Bayern Christian Lell

Capristo is Ozil's girlfriend but he has been accused of cheating on her by German Lell
Capristo ni mpenzi wa Ozil lakini ametuhumiwa juu ya usaliti na Lell
Lell, pictured with Melanie Rickinger during a restaurant opening in Munich in September, has accused Ozil
Lell, akiwa katika picha na Melanie Rickinger wakati wa ufunguzi wa mgahawa mjini Munich mwezi Septemba, amemtuhumu Ozil

'Mesut ametumia umaarufu wake na kunitunishia misuli juu ya mahusiano yake na mpenzi wangu,' amesema Lell. 'hiyo si sawa'.
Ozil mwenyewe amekataa kuzungumzia lolote juu ya hilo. 
'hatusemi lolote juu ya hilo. Tunaendelea kungalia mambo yanavyokwenda, na kuchukua hatua za kisheria kama itakuwa muhimu,' Amesema wakala wa mchezaji Ozil Roland Eitel. 

Kwa upande wa mpenzi wa zamani wa nyota wa soka Lell, Rickinger amenukuliwa akisema mpenzi wake huyo wa zamani ni mwendawazimu . Hata hivyo hakukanusha juu ya shutuma hizo za kuwa na mahusiano na Ozil, lakini amesisitiza kuwa Lell amefuatialia jumbe hizo bila ya ruhusa yake.
'Nilifuta kila kitu katika simu yangu. Atakuwa amefuatilia kila kitu, ni wazi kabisa ni mwendawazimu.'

Ozil, in action for Arsenal against Chelsea earlier this month, is accused of having an affair


Lell (right), pictured celebrating with Hertha Berlin in 2011, used to play for Bayern Munich
Lell (kulia), pichani anaonekana akishangilia akiwa na kikosi cha Hertha Berlin mwaka 2011, aliwahi pia kuichezea Bayern Munich

Mpenzi wa sasa wa Ozil Capristo hakuwa tayari kuweka maoni yake juu ya hilo. Mwanamuziki huyo kwasasa anaishi na nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani jijini London, na anafanya kazi ya jaji katika onyesho la kusaka nyota maarufu la 'X Factor-style reality show' nchini Ujerumani.
Ozil talks to Capristo after Germany's World Cup final victory over Argentina in Brazil
Ozil akiongea na Capristo baada ya mchezo wa fainali ya kombe la dunia dhidi ya Argentina nchini Brazil
Capristo is a judge on German X Factor-style show 'Germany's Search for a Superstar'
Capristo akiwa kazini kama jaji katika onyesho la German X Factor-style nchini Ujerumani wakisaka Superstar'

No comments:

Post a Comment