KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 2, 2010


kenya wazoa medali
Matukio ya kukumbukwa
Yator’s atereza na kumpa nafasi Soi kushinda mbio za mita 5000m
Tukio amblo halisahaulika kwa watazakaji wa mbio za mwaka huu huko kenya ni pamoja na mbio za mita 5000 pale ambapo mwanariadha aliyekuwa akiongoza mbio hizo kwa muda mrefu wa mbio hizo alipotereza katika zikiwa zimesalia mita kumi kumalizika kwa mbio Vincent na kumruhusu mpinzani wake wa karibu katika mbio hizo anayeshikilia medali ya shaba ya michuano ya Olimpik Edwin Soi kupata nafasi ya kutwaa medali ya dhahabu na kuipa kenya medali nyingine ya dhahabu katika na kujiongezea idadi ya medali.
Baada ya kuanza taratibu katika mzunguko wa kwanza alianza kuchukua nafasi ya kuongoza baada ya mzunguko wa tatu wakati ambapo mganda Moses Kipsiro ambaye alishinda medali ya silver katika mbio za mita 10,000 siku ya ufunguzi alipokuwa akiwaongoza wapinzani wake watatu kwa umbali mkubwa wa karibu hatua 26.

Hata hivyo Yator,ambaye alimaliza katika nafasi ya sita katika mbio za dunia za vijana “World Junior Championships” za mita 5000 huko Bydgoszcz nchini Poland miaka miwili iliyopita alipokuwa akijaribi kupunguza mwanya katika mbio za mita 3000 ushindani ukiwa ni kati yake na Kipsiro pamoja na Soi na Mark Kiptoo wakiwa mbele ya waethiopia Tariku Bekele na Imane Merga.
Katika mbio za mwaka huu licha ya tanzania kujiandaa kwa muda mrefu lakini mbinu za michezo kwa timu ya tanzania katika mbio tofauti tofauti ilikuwa ni tatizo kiasi kuifanya kurejea nyumbani bila ya hata medali moja katika mbio hizo za 17 za Afrika na mara hii zikiandaliwa nchi jirani ya Kenya.
Tukio lingine ambalo halitasahaulika ni kwa mwanariadha wa kike wa tanzania kuanza mbio ndefu za mita 10,000 kwa kuanza kutimua mbio tangu mapema na kufanikiwa kuongoza mpaka mzunguko wa tatu una malizika bila kujua mbio hizo zina safari ya kuzunguka uwanja mara 25.
Hakufika mbali baada ya mizunguko hiyo mitatu pale alipoanza kuchoka na wanariadha wenye majina kuanza kumpita mmoja baada ya mwingine na kumzunguka tena na tena na kupoteza matumaini ya watanzania katika mbio hizo .Swali nini sababu ya watnzania kushindwa kufurukuta katika mbio hizo mmoja wa viongozi alipoongea nami anasema hakukuwa na maandalia ya kutosha.

No comments:

Post a Comment