KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 25, 2012

Mashindano ya 126 ya Wimbledon yameanza




Li Na raia wa China aliye anza vizuri Wimbledon
Mashindano ya tennis ya Wimbledon nchini Uingereza yameanza hii leo huku wachezaji mahiri wanaoshiriki wakiwemo kama Novak Djokovic kutoka Jamhuri ya Serbia, Maria Sharapova ambaye ni raia wa Urusi na Roger Federer kutoka Uswisi.
Kati ya wachezaji ambao mambo yameanza kuwaendea vyema hii leo ni Mchina Li Na, ambaye moja kwa moja ameingia raundi ya pili ya mashindano, kwa kumuondoa Ksenia Pervak wa Kazakhstan 6-3, 6-1.
Baada ya kuondolewa mapema katika mashindano ya French Open katika raundi ya nne, Li Na anaonekana ameongeza juhudi za kufanya vyema katika mapambano ya Wimbledon.
Hata hivyo alimzidi nguvu Pervak, mwenye umri wa miaka 21, na kumfunga mapema akitumia muda chini ya saa moja.
Sasa Li Na atakutana na Sorana Cirstea kutoka Romania, au Mfaransa Pauline Parmentier, katika raundi ya pili.
Venus Williams aanza hovyo mzunguko wa kwanza wa Wimbledon
Venus Williams akifuta machozi baada ya kuharibu round ya kwanza Wimbledon
 Bingwa mara tano wa michuano ya Wimbledon Venus Williams anasema hafikiriii kuacha kucheza licha ya kupata kichapo cha kwanza mshituko toka kwa Elena Vesnina katika mzunguko wa kwanza wa michuano hiyo.
Mmarekani huyo mwenye umri wa miaka 32 ambaye alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Sjogren's Syndrome(hali ya kuwa na maumivu katika nyama na mwili kukauka) alifungwa kwa 6-1 6-3 na raia wa Russian Elena ambaye ni namba 79 kwa ubora duniani.
Amenukuliwa akisema
"haiwezekani nakwenda kufikria na kupiga moyo konde"
Williams alimudu kuzuia mara moja tu na kutupa hovyo katika set ya kwanza.

No comments:

Post a Comment