KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, July 5, 2012

ROBIN VAN PERSIE AWAVURUGA WAMILIKI ARSENAL


Alisher Usmanov bilionea mmiliki wa hisa Arsenal
Mwanahisa wa pili kwa ukubwa wa hisa yake katika klabu ya Arsenal Alisher Usmanov amekosoa uendeshwaji wa klabu hiyo baada ya Robin van Persie kutangaza kuwa hana mpango wa kuongeza mkataba ndani ya klabu hiyo.
bionea huyo raia wa Uzbektan ameitumia barua yenye maneno makali bodi ya klabu hiyo akiwashutumu kwa kukosekana uwekezaji ndani ya klabu hiyo.
"bado kwa mara nyingine tunakabiliwa na kupoteza wachezaji wetu wa ukweli mwenyewe akitumia neno ‘true marquee’ kwasababu hatuwezi kuwapa hali ya kujiamini kwao kuwa tunaweza kushinda mataji.
“kama klabu kubwa tuanapaswa kwa dhati kabisa kulingana au kushinda offer za klabu nyingine kwa kujaribu kuwapa mazingira mazuri wachezaji wetu wazuri na kuwajengea mustakabali mzuri wa baadaye”
 Usmanov ambaye ana miliki kampuni ya Red and White Holding company anamiliki hisa ya asilimia 29% ndani ya klabu hiyo . mfanya biashara wa kimarekani Stan Kroenke mwenye umri wa miaka 64 ndiye anae ongoza katika ukamataji wa hisa katika klabu kubwa za ligi kuu ya nchini Uingereza akimiliki asilimia 63% ya klabu hiyo.
Kroenke alijaribu kutaka kukamilisha umiliki wa hisa katika klabu hiyo mwaka 2011 lakini  Usmanov mwenye umri wa miaka 58 alisisitiza kutokuwa tayari kuuza hisa yake hiyo.
Mshambuliani Van Persie mwenye umri wa miaka 28, ambaye amebakiza mwaka mmoja katika maktaba wake hapo jana alitanabaisha kuwa yeye, meneja Arsene Wenger na mtendaji wa klabu Gazidis walishindwa kukubaliana jinsi ambavyo klabu itaendelea katika siku za usoni.

No comments:

Post a Comment