KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, March 20, 2013

SAMATA, ULIMWENGU WAANZA MAZOEZI BAADA YA KURIPOTI KAMBINI

Masoud Nassor Cholo na Salum Abubakar sureboy katika mazoezi ya timu ya timu ya taifa yaliyofanyika uwanja wa taifa jana jioni(picha kutoka lenzi ya michezo).
 Masoudi Nassoro na Mbwana Samata wakifanya mazoezini uwanja wa jana Taifa.
Washambuliaji wa Taifa Stars, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wameanza mazoezi na timu ya taifa baada ya kuwasili nchini tayari kwa maandalizi ya mchezo wa kundi C dhidi ya Morroco utakao fanyika jumamosi uwanja wa taifa.
Ujio wa washambuliaji hao unafanya idadi ya wachezaji walioripoti kambini kufikia 20 kati ya 23 walioitwaa baada ya mshambuliaji Khamis Mcha aliyekuwa na kikosi cha timu yake ya Azam nchini Liberia naye kuripoti kambini leo asubuhi.

Wachezaji John Bocco na makipa Mwadini Ally na Aishi Manula ambao pia nao walikuwa Liberia na timu yao ya Azam wataripoti kambini leo alasiri. Wachezaji hao ni sehemu ya msafara wa timu ya Azam ambao utakuja na ndege ya mchana kutokea Nairobi kwa vile ile ya asubuhi waliyotangulia nayo wenzao kuwa imejaa.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha Kim Poulsen jana imeendelea na mazoezi Uwanja wa Taifa. 

No comments:

Post a Comment