KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, January 15, 2014

Aston Villa wamemchukua straika Grant Holt kwa mkopo kutoka kwa Wigan

Aston Villa wamemchukua straika Grant Holt kwa mkopo kutoka kwa Wigan Athletic kwa kipindi cha msimu kilichosalia.
 Klabu hiyo inayoshiriki Ligi ya Premia imesema hayo kupitia tovuti yake ya klabu.
Holt, ambaye alijiunga na mabingwa wa sasa wa Kombe la FA Wigan mwaka uliopita akitokea Norwich City, amejiunga tena na meneja wake wa zamani Paul Lambert.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye alifunga mabao 53 katika mechi 92 alizochezea Norwich, amechukuliwa na Villa kujaza pengo lililoachwa na Libor Kozak ambaye ni majeruhi.
"Kumpoteza Libor kutokana na jeraha ni pigo kwetu, bila shaka. Nilipojua kwamba Grant alikuwa amewekwa sokoni nilitaka haraka kumchukua kwa sababu ataongeza nguvu na uzoefu katika kikosi chetu ambacho kwa jumla bado kinahitaji mabadiliko” Lambert aliambia avfc.co.uk.
"Ninajua yale anaweza kufanya na hilo ni muhimu.”
Villa wako nambari 11 katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza, alama tano kutoka eneo la kushushwa ngazi na wametatizika katika kufunga mabao msimu huu. Wamefunga mabao manane pekee nyumbani msimu huu.
"Kuweza kurudi tena katika Ligi ya Premia, hasa katika klabu kubwa kama Villa, ni jambo kubwa kwangu na fursa kwangu kufanya kazi tena na meneja wangu wa zamani na watu wake," Holt alisema.
"Sote tunafahamu kwamba hii ni klabu iliyo katika mpito lakini tunapiga hatua. Tuna vijana wengi wachanga kwenye klabu ambao wanafanya kazi nzuri na nina furaha kujiunga nao na kuweza kusaidia,” akaongeza.

No comments:

Post a Comment