KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 24, 2012

HABARI MBALIMBALI KIMATAIFA:Cazola kwenda Arsenal,Mourinyo apata mrithi Inter,Dani Alves anasema Barca ilimchanganya,Ryan Babel aondoka kwa aibu Hoffenheim na nyinginezo.

Cazorla mguu ndani mguu nje kwenda Arsenal
Santi Cazorla
Arsenal huenda ikamsajili winga Santi Cazorla toka katika klabu ya Malaga ambayo inakabiliwa na tatizo kubwa la kifedha ambapo imeelezwa kuwa Arsenal imeshakubali kutoa euro milioni €20 kama ilivyo ripotiwa kuwa tayari kuna makubaliano yameshafikiwa juu ya kumchukua nyota huyo wa kimataifa wa Hispania.
Cazorla mwenye umri wa miaka 27 alikuwa kwenye mipango ya Arsenal tangu msimu uliopita lakini Malaga iligomea mpango huo tofauti na sasa ambapo kuna kila dalili za klabu hiyo ya nchini Hispania kumtoa winga huyo licha ya kuendelea kuweka pingamizi.
Winga huyo ameripotiwa na gazeti la Guardian kuwa amefanya mazungumzo na Malaga na kuwaeleza kuwa anatamani kuondoka na kuijulisha Arsenal kwamba angependa kueleka kaskazini mwa London.
Mazungumzo kati ya vilabu hivyo yanaarifiwa kufanyika katika Talks between the clubs are reported to have taken place against a backdrop of increasing financial
Hali ya sintofahamu imeingia katika klabu ya Malaga ambayo tayari taarifa zake zimesha pelekwa katika chama cha wachezaji soka nchini Hispania (AFE) na wachezaji wanne akiwemo Cazorla mwenyewe kuwa wamekuwa hawana mshahara.
Chini ya Under sheria mpya ya iliyotolewa mwezi April, kklabu hiyo inatakiwa mpaka kufikia Julai 25 iwe imetoa majibu ya malalamiko hayo na mpaka kufikia mwisho wa mwezi kuwa imefikia makubaliano na wachezaji wake juu ya tatizo hilo.
Kushindwa kufanya hivyo kunaweza kunaweza kuwashusha daraja na kuondoshwa katika ligi ya mabingwa.
Cazorla alijiunga na Malaga akitokea Villarreal kwa uhamisho wa euro €19 majira ya kingazi yaliyopita na baada ya msimu huu amekumbwa kadhia ya kukosa mshahara ikiwa ni pamoja na bonas zake kiasi kutamka kutaka kuondoka.

Sneijder: Stramaccioni ndiye bora baada ya Mourinho

Stramaccioni
Wesley Sneijder
Wesley Sneijder anaamini kuwa Andrea Stramaccioni ndiye mtu muafaka kuisaidia Inter kurejea kileleni baada ya kuvurunda katika kampeni ya 2011-12.
kocha huyo mwenye umri wa miaka 36 ameanguka saini ya kupiga kazi ya kufundisha kwa mkataba wa kudumu kama kocha wa Nerazzuri majira haya ya kiangazi  baada ya aliyekuwa akifanya kazi hiyo kwa mkataba wa muda mfupi baada ya Claudio Ranieri.
Sneijder ana matumaini kuwa bosi huyo kijana ni mtu sahihi kwa kazi hiyo pale Inter baada ya kuondoka kwa  Jose Mourinho.
amenukuliwa akisema
"Stramaccioni ndiye bora kwa Inter baada ya Mourinho,".
"klabu hii inajenga mustakabali wa baadaye na Stramaccioni ndiye kocha wa mpango huo hapa Inter katika kipindi hiki. ana mpango mkubwa na timu hii"
Sneijder alikuwa chini ya Mourinho katika miaka ya 2009 na 2010.


Alves: Barca ilinichanganya
Dani Alves
 Mlinzi wa Barcelona Dani Alves ameweka wazi kuwa alichanganywa na klabu hiyo kwa kushindwa kukanusha tetesi za yeye kutaka kuondoka.
Alves mwenye umri wa miaka 29 alihusishwa na kutaka kuhamia katika klabu za Anzhi Makhachkala na Manchester City mapema katika majira haya ya uhamisho wa kiangazi lakini Barcelona haikuchukua hatua zozote za kukanusha habari hizo za kuwepo mazungumzo ya yeye kweli kutaka kuondoka.
Mlinzi huyo raia wa Brazil katika kipindi hicho alikuwa akidhani kuwa klabu yake maarufu kama Blaugrana ingekanusha taarifa uvumi huo.
amenukuliwa akisema
"ni kweli kulikuwepo uvumi kuwa sitakuwepo  Barca na nilichanganyikiwa na klabu yangu haikuingilia kati,"
"hata hivyo naona niko juu ya hilo na kama wakati utawadia na kama klabu yangu itakuwa hainihitaji tena nitakubaliana na hilo na nitaondoka kama ilivyokuwa wakati najiunga nayo."
Alves alijiunga na Barcelona kwa ada ya kushitua ya euro milioni €35.5 mwaka 2008 baada ya kutoa huduma katika klabu ya Sevilla ambayo ilishinda mataji mawili ya UEFA Cup , na Copa del Rey.

Maamuzi ya Hoffenheim kumuacha Babel ni kinyume cha mkataba
Ryan Babel

Kitendo cha kuondoka kwa Ryan Babel toka katika klabu ya Hoffenheim kimeelezwa kuwa kimekwenda kinyume na taratibu za kimkataba kwa mduchi huyo. Kauli hiyo imetolewa na wakala wa mchezaji huyo.
Kocha Markus Babbel amenukuliwa akisema kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 25 pamoja na Edson Braafheid wanaweza kuondoka Rhein Neckar Arena na kumkosoa zaidi mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool kwa kiwango kibovu alicho onyesha tangu ajiunge na klabu hiyo January 2011.
Hata hivyo wakala wake Babel , Winnie Haatrecht, amesisitiza kuwa sababu zinazo tolewa na Hoffenheim kumruhusu mshambuliaji huyo kuondoka na mbaya kabisa kumfukuza mpaka kambini ni kinyume mambo yaliyomo ndani ya mkataba.
Amenukuliwa Haatrecht akiongea na De Telegraaf akisema
"katika kipindi cha uhamisho wa dirisha dogo tuliingia katika makubaliano ya kimkataba na Hoffenheim. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na mshahara wa Ryan kuongezwa mara mbili endapo atacheza michezo angalau michezo minne msimu ujao"
"jambo la kushangaza ni kuwa , Hoffenheim imemuondosha katika orodha yao wakati ambapo bado ana mwaka mmoja katika mkataba wake.
"leo hii , Ryan wanataka afanye mazoezi na kikosi cha kiba, inabidi asubiri. haitakuwa rahisi kwake kupata uhamisho, kwasababu Hoffenheim haitaki hata kuwepo na uhamisho wa mkopo.

Yanga-Mbiwa anafikiria juu ya hatma yake ya baadaye

Mapou Yanga-Mbiwa
 Mapou Yanga-Mbiwa amekuwa akifikiria kuondoka Montpellier licha ya Rais wa klabu hiyo Louis Nicollin, akionekana kwenda tofauti na mawazo hayo.
AC Milan imekuwa ikivutiwa na mlinzi huyo Yanga-Mbiwa mwenye umri wa miaka 23 ili kuziba nafasi ya Thiago Silva, lakini Nicollin ameonya
 "Yanga-Mbiwa hataondoka” .
"ili kuwa na makubaliano zaidi na Milan, tungehitaji kuwa na makubaliano zaidi.  Hatuna makubaliano hivyo hakuna makubaliano ya kueleweka.
"najua kuwa wametoa offer ya euro milioni €6 lakini hata kama wataongeza mara tatu ya hiyo bado haitoshi na mbaya zaidi sina mbadala wake, kwa hiyo ni wazi kuwa hataondoka. Haijalishi hata kama yuko ukingoni mwa mkataba wake."
Lakini wakati hayo yakiendelea mchezaji mwenyewe amekuwa akisisitiza kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuondoka majira haya ya uhamisho wa kiangazi.

No comments:

Post a Comment