KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 16, 2012

MWENYEKITI WA SIMBA ISMAIL RAGE KUREJEA NYUMBANI USIKU HUU.


Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage
Hali mwenyekiti wa simba wa klabu ya simba Ismail Aden Rage imeelezwa kuendelea vizuri na anatarajiwa kuanza safari ya kurejea nchini usiku huu.
Rage aliondoka nchini kuelekea India kwa ajili ya matibabu ya mgongo uliokuwa unamsumbua amefanikiwa kufanyiwa upasuaji mdogo na kwasasa yuko katika hali nzuri kuweza kurejea nchini kuitumikia klabu yake ya Simba ,familia yake na wananchi wa Tabora mjini.
Akiongea na Rockersports makamu mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange Kaburu amesema wanatarajia kuwa na mwenyekiti wao hapo kesho endapo mungu atamfikisha nyumbani salama.
“ripoti ya daktari inaonyesha kuwa mwenyekiti wetu amepata nafuu baada ya upasuaji mdogo aliofanyiwa na anaanza safari ya kurejea nyumba usiku huu”

No comments:

Post a Comment