KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 31, 2012

ARGENTINA YATANGAZA KIKOSI DHIDI YA SAUDI ARABIA NA VILLA ANASEMA ANATAKA NAMBA YA KUDUMU BARCA LAKINI ................


Bosi wa kikosi cha timu ya taifa ya Argentina Alejandro Sabella ametaja kikosi cha wachezaji 23 kitakacho pambana na kikosi cha kocha Frank Rijkaard cha timu ya taifa ya Saudi Arabia mchezo ambao unatarajiwa kuchezwa katika mji wa Riyadh.
Lionel Messi, Angel Di Maria, Javier Mascherano na Gonzalo Higuain wameendelea kuwemo katika mpango ya bosi huyo lakini pia akiwajumuisha wachezaji wengine kadhaa wakiwa ni sura mpya kabisa katika kikosi cha timu hiyo.
Nyota wa Wigan  Franco Di Santo ameingizwa kikosini ikiwa ni mara ya kwanza kujumuishwa katika kikosi cha timu hiyo na amepata nafasi hiyo baada ya kuonyesha uwezo katika michezo ya mapema ya kuanza msimu wa ligi kuu ya England ‘Premier League season’.
Ricky Alvarez wa Inter Milan ya Italia amejumuishwa akichukua nafasi ya Erik Lamela wa Roma, wakati ambapo Fabian Rinaudo, Cristian Alvarez na Tino Costa kwa pamoja wakijumuishwa kwa mara ya kwanza.

Baada ta kushinda michezo ya kampeni ya kufuzu fainali ya kombe la dunia dhidi ya Uruguay na Chile vijana hao watataka kushinda pia mchezo huu wa tatu mfululizo kudhihirisha ubora wa kikosi chao.
Kikosi kizima
Walinda milango:         
Sergio Romero-Sampdoria
Mariano Andujar-Catania
Cristian Alvarez-Espanyol
Walinzi:  
Hugo Campagnaro -Napoli
Pablo Zabaleta -Manchester City
Marcos Rojo-Sporting Lisbon
Federico Fernandez-Napoli
Ezequiel Garay-Benfica
Luciano Monzon-Lyon
Fabricio Coloccini-Newcastle
viungo:    
Fernando Gago-Valencia
Javier Mascherano-Barcelona
Angel Di Maria-Real Madrid
Augusto Fernandez-Celta Vigo
Enzo Perez-Benfica
Tino Costa-Valencia
Ricky Alvarez-Inter
Fabian Rinaudo-Sporting Lisbon
washambuliaji:      
Lionel Messi -Barcelona
Sergio Aguero-Manchester City
Gonzalo Higuain-Real Madrid

Eduardo Salvio-Benfica
Franco Di Santo-Wigan

Sammer amekosea kwenda mbele ya jamii kuikosoa Bayern, anasema Jens Lehmann.
Mlinda mlango wa zamani wa kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani Jens Lehmann amemkosoa mkufugenzi wa michezo wa Bayern Munich Matthias Sammer kufuatia maoni yake ya hivi karibuni kuwa amehuzunishwa na kiwango duni kinachoonyeshwa na wachezaji wa timu hiyo.
Sammer ametoa kauli ya kuonyesha kutokupendezwa na kiwango cha hovyo kinachoonyeshwa na mabingwa wa Bundesliga kutokana na kichapo kutoka kwa BATE Borisov katika ligi ya mabingwa Ulaya licha ya ushindi wao dhidi ya Werder Bremen, na Lehmann anaamini kuwa nyota huyo wa zamani wa Borussia Dortmund ameenda mbali sana.
"sidhani kama atakurupuka na kuzungumza juu ya kiwango cha Bayern katika vyombo vya habari tena.
Hata hivyo nyota huyo wa kimataifa wa zamani wa ujerumani akaenda mbele zaidi kwa kusema maoni ya Sammer yana haribu taswira ya klabu
"hakutakiwa kwenda kusema kitu kama hiki mbele ya umma kwasababu kufanya hivyo ni kumaanisha Bayern imepoteza heshima yake”
David Villa: Nataka namba ya kudumu Barca lakini.....
David Villa ana matumaini makubwa ya kupata muda mwingi wa kucheza katika klabu yake ya Barcelona, lakini pia anakubali hilo si jambo rahisi kwa kuwa anakabiliwa na ushindani mkubwa wa kupata namba katika kikosi cha kwanza ndani ya klabu hiyo.
Villa mwenye umri wa miaka 30 alikuwepo katika kikosi kilicho anza jumanne ya jana ambapo Barca uliibuka na ushindi wa mabao 3-0 mchezo wa Copa del Rey dhidi ya Alaves, na alifanikiwa kufunga goli safi ambalo lilimrejesha katika matumaini zaidi.
"kama ilivyo kwa mcheza soka yoyote nataka kucheza mara nyingi kwa kadri ya uwezo wangu wote,".
"nacheza katika klabu bora duniani na changamoto ya kupata namba ni kubwa. tunacheza michezo mingi na kuna mashindano mengi.
Barcelona itarejea katika ligi kuu jumamosi ambapo watakuwa wenyeji wa Celta Vigo.

No comments:

Post a Comment