KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 31, 2012

LIGI YA SOKA TANZANIA BARA: YANGA HABARI NDIYO HIYO, SIMBA YATOROKEA MLANGONI KWA POLISI.


Beki wa Yanga ,Nadir Haroub (kulia) akifunga goli la kwanza,huku wachezaji wa JKT Mgambo ,Salum Kipanga (19) na Ramadhani Malima wakiwa hawana la kufanya katika mechi ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kulia ni Vicent Pius.Yanga ilishinda
Beki wa Yanga ,Nsajigwa (katikati) akiwatoka wachezaji wa JKT Mgambo,Yasin Awadh (namba 22) na Fully Maganga katika mechi ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

Simon Msuva (kulia) akijaribu kumpiga chenga beki wa JKT Mgambo Salum Kipanga.
Nadir Haroub Kanavaro akifurahia bao lake la kwanza katika mchezo wa ushindi kwa Yanga wa mabao 3-0.
Mbuyu Twite akimpaka upako Kanavaro baada ya kufunga bao la kwanza katika mchezo dhidi ya Mgambo JKT.
Mshambuliaji wa Yanga Didier Kavumbaguakijaribu kumtoka mlinzi wa Mgambo.
Ligi kuu ya soka Tanzania Bara imeendelea tena hii leo kwa michezo minne kuchezwa katiika viwanja vinne tofauti hapa nchini.
Katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Yanga walikuwa wenyeji wa JKT Mgambo mchezo ambao umemalizika kwa Yanga kupata ushindi wa mabao 3-0 huku mabao yakifungwa Nadir Haroub Kanavaro akifunga bao la kwanza kwa kichwa baada ya mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na kiungo Athumani Iddi Chuji.

Bao la pili lilifungwa na Didier Kavumbagu kufuatia pasi safi ya Hamisi Diego Kiiza na bao la tatu likifungwa na Jerson Tegete baada ya kupokea mpira mrefu wa mlinzi wa pembeni Oscar Joshua.

Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha alama 23 sawa na kinara wa ligi hiyo Simba ambaye alikuwa akiongoza ligi hiyo kwa muda mrefu tangu kuanza kwa ligi.

Wao Simba wakiwa katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro wamekwenda sare ya bao 1-1 na polisi ya huko matokeo ambayo yamewasononesha mashabiki wa Simba ambao walikuwa wakihitaji ushindi na timu ambayo imekuwa kibonde katika ligi na ambayo haijawahi kushinda hata mchezo mmoja tangu kuanza kwa ligi.

Matokeo hayo yanaifanya Simba iendelee kuongoza ligi kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa ambapo Simba ina mabao 20 ya kufunga huku ikifungwa jumla ya mabao 8 na hivyo ikiwa na uwiano wa mabao 12( goal difference 12), ambapo Yanga ina mabao ya kufunga 21 huku ikiwa imefungwa mabao 10 ambapo itakuwa na uwiano wa mabao 11(goal difference 11)
(Tazama msimamo kulia) 
Kikosi cha Simba
Mchezo mwingine ulikuwa ukichezwa katika uwanja wa Chamazi Complex ambapo Afrikan Lyon ilikuwa mwenyeji wa JKT Ruvu na matokeo ya mchezo huo ni kwamba JKT Ruvu imeichapa Lyon kwa mabao 4-2.

Mtibwa Sugar wakiwa katika uwanja wao wa Manungu imefanikiwa kuichapa JKT Oljoro ya Arusha mabao 2-1.

Ratiba michezo ijayo
Kesho.
Azam vs Coast Union (Chamazi Complex) 
Toto Afrikans vs Kagera Sugar (CCM Kirumba Mwanza)

Mzunguko wa 1

NO DATE No.  HOME TEAM AWAY TEAM STADIUM VENUE
12 03.11.2012. 82 RUVU SHOOTING TOTO AFRICANS MABATINI PWANI
03.11.2012. 78 AFRICAN LYON MGAMBO JKT AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
07.11.2012. 79 MTIBWA SUGAR JKT RUVU MANUNGU MOROGORO
03.11.2012. 81 KAGERA SUGAR TANZANIA PRISONS KAITABA KAGERA
03.10.2012. 80 YOUNG AFRICANS SIMBA NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
07.11.2012. 83 AZAM JKT OLJORO AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
07.11.2012. 84 COASTAL UNION POLISI MOROGORO MKWAKWANI TANGA

  

No comments:

Post a Comment