KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, October 26, 2012

Silvio Berlusconi kwenda jela miaka minne kwa kukwepa kodi.




Waziri mkuu wa zamani wa Italia ambaye pia ni Rais wa klabu ya AC Milan ya nchini humo Silvio Berlusconi amehukumiwa kwenda jela miaka minne kutoka na ukwepaji wa kodi.

Berlusconi na wenzie 10 walikuwa wakituhumiwa kununua haki za kampuni ya kimarekani ya filamu kwa bei ya kutupa kupitia kampuni za nje wakati wa utawala wake kama waziri mkuu.

Waziri huyo mkuu wa zamani wa Italia anatarajiwa kukata rufaa juu ya hukumu hiyo.

Katika usomwaji wa hukumu hiyo aliunganishiwa kesi mbalimbali zinazohusu mambo ya kibiashara lakini zilitupiliwa mbali kwa kigezo cha kwamba zilikuwa nje ya muda.

Wakati akisomewa hukumu hii , waendesha mashitaka walidai kuwa sehemu ya pesa za kununulia haki za filamu zilitumika katika uharamia wa kukwepa kodi kupitia kampuni yake ya Mediaset.

Mahakama imemuhuku Berlusconi muda mrefu jela kuliko miaka mitatu na miezi nane kama ilivyoombwa na waendesha mashtaka.
Habari zaidi zinakuja

No comments:

Post a Comment