KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, November 5, 2012

Yaya Toure: Nataka kumalizia soka Manchester City, Luis Suarez ndiye Lionel Messi wa Liverpool anasema Brendan Rodgers, Shearer: Arsenal inaendelea kutereza NA tuzo za ubora Afrika Yaya Toure ndani na Katongo wa Zambia.



Kiungo wa Manchester City Yaya Toure amesema lengo lake ni kumalizia soka yake katika klabu yake ya sasa ya Manchester City ambao ndio mabingwa soka nchini England.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 raia wa Ivory Coast amekuwa kivutio kikubwa cha kocha Roberto Mancini tangu kuwasili kwake ndani ya klabu hiyo mwaka 2010 akitokea kwa kigogo cha nchini Hispania Barcelona.

Amenukuliwa Toure alipokuwa akiongea na gazeti la L’Equipe akisema,
"katika maisha sio pesa tu, lakini pia wazazi na familia, tangu niwasili hapa nimekuwa nikipata mshahara mzuri lakini si kwamba napata kila kitu".

"kwa kuwa nimetokea katika klabu ya Barcelona nikiwa na historia nzuri  nikafika City kwa umuhimu mdogo, lakini kitu kimoja ambacho nakitaka ni kuandika ni historia. Naweza kuweka historia hapa City. Nina uhakika na hilo nitakapo kuwa mtu mzima watu siku moja watanizungumzia.

"nataka kumalizia soka yangu Manchester City kwa heshima kutoka kwa mashabiki lakini katika soka huwezi kujua ya baadaye."

Luis Suarez ndiye Lionel Messi wa Liverpool anasema Brendan Rodgers

Bosi wa Liverpool ya nchini England Brendan Rodgers amemuelezea mshambuliaji wake Luis Suarez kuwa anafanana na kiuwezo Lionel Messi baada ya kuonyesha soka safi katika mchezo dhidi ya Newcastle.

Suarez alifunga goli zuri la kusawazisha katika mchezo huo huku akionyesha kiwango safi ndani ya muda wote wa mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 mchezo aambao ulipigwa Anfield.

Amenukuliwa Rodgers na Sky akisema,
"amecheza kwa majukumu nane tofauti ndani ya kiwanja kama anavyo fanya Messi katika klabu yake ya Barcelona ambaye anatembea akiwa huru uwanjani na wengine wakimfuata nyuma kujaribu kupenya".

"goli la Suarez lilikuwa goli safi la kupendeza. Ni mshambuliaji wa kiwango cha dunia."

Suarez alikuwa tishio kubwa wakati wa mchezo huo akiwapa tabu wapinzani sehemu yao ya ulinzi na kiungo huku utembeaji wake uwanjani na upenyeshaji wake wa mipira ukiwapa tabu wapinzani.

Shearer: Arsenal inaendelea kutereza.

Alan Shearer amelaumu kiwango kibovu cha Arsenal walicho kionyesha katika mchezo dhidi ya Manchester United na kudokeza kuwa klabu hiyo si muda mrefu itapoteza hadhi yake kama klabu kubwa ya kuogopa duniani hasa kutokana na rekodi yake mbaya ya hivi karibuni.

Kipigo kutoka kwa United kilikuwa ni kipigo cha tatu katika msimu huu wa ligi huku mshambuliaji wake wa zamani Robin van Persie akifunga goli la uongozi baada ya kufanyika makosa yaliyosababishwa na mlinzi Thomas Vermaelen.

Amenukuliwa Shearer na The Sun akihoji
"hivi ni klabu gani duniani itaendelea kukaa na meneja ambaye hana taji hata moja ndani ya kipindi cha miaka saba na nusu? Au ni Arsenal pekee inayojiweka katika kundi la kipekee".

"mnafarijika kuona wachezaji bora wakiondoka katika mazingira ambayo mna uwezo nayo, hii inatisha na mbaya zaidi hakuna wakuchukua nafasi yake."

Shearer anaamini kuwa Theo Walcott atafuata nyayo za nyota wengine wakubwa ambao waliihama klabu hiyo ndani ya kipindi cha miaka minne iliyopita.

Ameendelea kwa kusema
"watu kama Van Persie, Cesc Fabregas, Samir Nasri, Gael Clichy, Kolo Toure na hivi punde atakuwa Theo Walcott. 

"Vina saba (DNA)  vimeondoka ndani ya klabu. Arsenal inaonekana kuporomoka katika hatua ambayo sasa wanaonekana kama si washindani tena wa mataji."

YAYA TOURE KUONGOZAORODHA YA KUWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA YUKO PIA KATONGO WA ZAMBIA

Cris Katongo nahodha wa Zambia.

Kiungo raia wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City Yaya Toure ni miongoni mwa wachezaji wanne wanaocheza soka nchini England waliotajwa kuwania tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika kwa mwaka 2012.
Kiungo wa Chelsea John Obi Mikel, mshambuliaji wa Arsenal Gervinho na mshambuliaji wa Newcastle United Demba Ba ni wachezaji wengine kutoka katika ligi kuu ya nchini England ‘Premier League’ waliojumuishwa.

Pia katika orodha hiyo kuna wachezaji wengine kadhaa walio wahi kucheza soka nchini  England mwaka huu wa 2012.

Wachezaji hawa ni pamoja na kiungo wa zamani wa Arsenal Alexandre Song, ambaye kwasasa anachezea Barcelona pamoja na mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Didier Drogba ambaye kwasasa anachezea klabu ya Shanghai Shenhua ya nchini China.

Chris Katongo ni mchezaji pekee kutoka kwa mabingwa wa soka barani Afrika Zambia.

Younes Belhanda raia wa Morocco naye ameorodheshwa katika orodha hiyo fupi kutokana na mchango wake mkubwa katika klabu yake ya nchini Ufaransa ya Montpellier ambayo inashiriki ligi soka ya nchi hiyo maarufu kama Ligue 1.

Wachezaji hao watapunguzwa mpaka kufikia watatu katika wiki ya mwisho ya mwezi Novemba.

Caf pia imetangaza orodha fupi ya wachezaji wanaocheza soka barani Afrika kwa ajili ya kuwania tuzo ya wachezaji wa ndani ya Afrika.

Miongoni mwao ni pamoja na kiungo wa Misri Mohamed Aboutrika, ambaye alicheza katika mchezo uliomalizika kwa sare ya 1-1 baina ya Al Ahly na Esperance ukiwa n I mchezo wa kwanza wa fainali uliopigwa jumapili.

Tuzo hizo pia zinajumuisha tuzo ya kocha bora na klabu bora ya mwaka ambapo sherehe za utoaji tuzo hizo ambazo zitafanyika Desemba 20 December katika ukumbi wa Banquet katika mji mkuu wa Ghana Accra.

Orodha kamili:
Alexander Song . Club: Barcelona (Spain) Country: Cameroon
Andre Ayew . Club: Marseille (France) Country: Ghana
Christopher Katongo. Club: Henan Construction (China) Country: Zambia
Demba Ba. Club: for Newcastle United (England) Country: Senegal
Didier Drogba. Club: Shanghai Shenhua (China) Country: Ivory Coast
Gervinho. Club: Arsenal (England) Country: Ivory Coast
John Obi Mikel. Club: Chelsea (England) Country: Nigeria
Pierre-Emerick Aubameyang. Club: Saint Etienne (France) Country: Gabon
Yaya Toure. Club: Manchester City (England) Country: Ivory Coast
Younes Belhanda. Club: Montpellier (France) Country: Morocco

Orodha ya wachezaji wanaocheza barani Afrika.

Mohamed Aboutreika. Club: Al-Ahly (Egypt) Country: Egypt
Rainford Kalaba. Club: TP Mazembe (DR Congo) Country: Zambia
Stoppila Sunzu . Club: TP Mazembe (DR Congo) Country: Zambia
Yannick N'Djeng. Club: Esperance Sportive de Tunis (Tunisia) Country: Cameroon
Yousse Msakni. Club: Esperance Sportive de Tunis (Tunisia) Country: Tunisia

No comments:

Post a Comment