KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, January 8, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA:Rosell anasema Villa hatoki kwa mkopo, Messi ame-share tuzo na Eric Abidal na Tito Vilanova na Demba Ba anasema Chelsea ikikosa taji la ligi ya Premier basi mataji mengine halili yao.

 Rais wa Barcelona Sandro Rosell mesema hakuna nafasi ya David Villa kuondoka Camp Nou kwa mkopo mwezi January.

Kutokana na mshambuliaji huyo kukosa nafasi katika kikosi cha Tito Vilanova msimu huu kimeibua tetesi nyingi juu ya kuondoka kwa mchezaji huyo na tayari vilabu mbalimbali hususani vya ligi kuu ya nchini England Liverpool, Chelsea, Arsenal na Spurs zikiripotiwa kumtaka mshambuliaji huyo mwenye rekodi ya ufungaji ya Hispania.

Hata hivyo Rosell akiongea na gazeti la ‘Catalan paper Sport’ hapo jana akiwa katika hafla ya utoaji wa tuzo za FIFA Ballon d’Or amesema mshambuliaji huyo haendo kokote.


Messi awashukuru Tito na Abidal
 Lionel Messi akitumia nafasi ya mahojiano yake na TV baada ya kutangazwa mshindi wa Ballon d'Or kwa mara ya nne mfululizo hakusahau kuwashukuru Tito Vilanova na Eric Abidal kutokana na mchango wao kwake.

Baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Messi aliwashukuru watu wengi ikiwa ni wachezaji wenzake wa klabu yake na timu ya faifa ambao walipiga kura kwake marafiki na mtoto wake mchanga.

Dakika chache baadaye akiongea na TV3 ya jijini Catalunya alionyesha wazi kuwashukuru kwa hisia kubwa kocha wake Barca Vilanova na Abidal ambao bado wanaendelea kuponya maumivu makali baada ya kuugua.

Amenukuliwa akisema

"kwa dhati kabisa ningependa kuchangia tuzo hii na Tito na Abidal, kilichotokea kwao ni pigo na kuwaona tunaungana tena tukifanya kazi pamoja inanipa furaha.

Hiyo ni tuzo kubwa kuwa wamerejea kuwa nasi tena. Kwasasa Tito anatakatiwa afanye kazi ya kurekebisha lakini bila shaka atakuwa vizuri, nilipokwenda kupokea tuzo hayo maneno yakuwa kichwani kwangu ".

Lionel Messi ameshinda tuzo hiyo ya Ballon d’Or baada ya kupata asilimia 41.60% ya kura zote akiwa mbele ya Cristiano Ronaldo aliyepata asilimia 23.68% na Andrés Iniesta akipata asilimia 10.91% ya kura zote.
Wambach, mshindi wa tuzo kwa upande wa wanawake aliingoza Marekani nchini Uingereza katika michuano ya Olympics 2012 jijini London, ambako huko alishinda tuzo ya mpira wa dhahabu ya kampuni ya Adidas ‘adidas Golden Ball’ kama mchezaji bora wa mashindano na pia tuzo ya ufungaji bora ya Adidas (adidas Golden Boot) baada ya kupachika wavuni jumla ya magoli 5. 
Amepata asilimia 20.67% ya kura zotr akiwashinda Mbrazil Marta na Alex Morgan kutoka Marekani ambao walipata asilimia 13.50% na 10.87% ya kura zote zilizopigwa.
Vicente del Bosque kama kocha bora wa timu ya za wanaume wa FIFA amepata asilimia 34.51% ya kura zote akiwashinda José Mourinho, kocha wa Ureno na klabu ya Real Madrid, aliyepata asilimia 20.49%, na kocha wa zamani wa FC Barcelona Pep Guardiola, aliyepata asilimia 12.91% ya kura zilizopigwa.
Wakati hayo yakiwa hivyo naye Pia Sundhage amekuwa kocha wa timu za wanawake wa mwaka baada ya kukusanya asilimia 28.59% ya kura zote akiwashinda Norio Sasaki wa Japan aliyepata asilimia 23.83%  aliyefanikiwa kupata medali ya fedha katika michezo ya Olympics jijini London, na kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa Bruno Bini aliyepata asilimia 9.02%.
FIFPro, muungano wa wachezaji wa duniani iliwaalika jumla ya wachezaji wakulipwa 50,000 kutoka sehemu mbalimbali duniani kuchagua timu bora ya mwaka 2012 (FIFA FIFPro World XI 2012). 
Waliochaguliwa ni pamoja na
Mlinda mlango -Iker Casillas (Spain)
Walinzi -Dani Alves (Brazil), Marcelo (Brazil), Gerard Piqué (Spain) na Sergio Ramos (Spain) 
Viungo-Xabi Alonso (Spain), Andrés Iniesta (Spain) na Xavi Hernández (Spain)
Washambuliaji- Cristiano Ronaldo (Portugal), Radamel Falcao (Colombia) na Lionel Messi (Argentina).
 Tuzo nyingine maarufu ilikuwa ni ‘FIFA Puskás Award’ ambayo inatoka kwa goli bora la mwaka ambayo inapigiwa kura kupitia mtandao wa FIFA ambapo goli hilo linawekwa katika mtandao wa FIFA.com kupitia YouTube na mtandao mwingine wa ‘francefootball.fr’ ambapo mashabiki zaidi ya milioni 5 wanawakilisha katika kulipigia kura goli hilo.
Tuzo hiyo kwa mara ya kwanza ilizinduliwa 2009 kwa heshima ya nyota na nahodha wa zamani wa Hungary Ferenc Puskás, ambaye alikuwa nahodha wa Hungary miaka ya 1950.

Kwa mara ya kwanza tuzo hiyo ilichukuliwa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Slovakia Miroslav Stoch, ambaye alifunga goli katika kisambusa cha ndani ya nyavu hiyo ilikuwa tarehe 3 March 2012 akiwa na klabu yake ya Fenerbahçe katika ligi kuu ya nchini Uturuki dhidi ya Gençlerbirliği.

Franz Beckenbauer amepewa tuzo ya heshima ya Rais wa FIFA Joseph S. Blatter katika kutambua mafanikio yake na rikodi yake nzuri katika soka kama mchezaji wa zamani lakini pia kama mshauri

Tuzo ya FIFA ya mchezo wa kiungwana ‘FIFA Fair Play Award ‘ imekwenda kwa shirikisho la soka la Uzbekistan (UFF).

Ba: Chelsea itatwaa mataji mengine.

Demba Ba amesisitiza kuwa ingawa Chelsea ina matumaini kidogo katika kuelekea kuchukua taji la ligi kuu ya nchini England, lakini bado wanapaswa kujitahidi ili kushindania mataji mengine.

Licha ya kwamba Chelsea ina mchezo mmoja mkononi ukilinganisha na vinara wa msimamo wa ligi Manchester United, hata hivyo Chelsea inahitaji miujiza kuvunja daraja kubwa la alama 14 kati yao.

Baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu na nusu wa kufanya kazi Stamford Bridge, Ba, mbaye alifunga magoli mawili katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Southampton katika michuano ya FA Cup, ameonekana kusema ukweli juu ya kile ambacho Chelsea inaweza kufanya msimu huu.

Akiongea na L’Equipe amesema

"ni ngumu kwetu kumkamata Manchester United anayeongoza ligi lakini bado kuna vikombe vitatu tunapaswa kujitahidi kushinda vikombe vingi ikiwezekana" Ba told L'Equipe.

No comments:

Post a Comment