KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, June 2, 2013

Entente Setif yafanya maajabu ya mwaka kombe la shirikisho na Neymar anasema jaribio la Ronaldo limeshindikana


Mabingwa wa soka nchini Algeria Entente Setif wamefanikiwa kufanya miujiza waliyokuwa wanaihitaji kuifunga US Bitam ya Gabon katika mchezio wa kusaka nafasi ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya vilabu ya kombe  la shirikisho barani Afrika.

Setif ilisafiri kuelekea Gabon ikiwa na kikosi cha wachezaji 14 wakiwemo walinda milango watatu kwa ajili ya mchezo wao wa mkondom wa pili. 

Wenyeji Bitam walishinda kwa mabao 2-0 hapo jana na kufanya matokeo kusimama 2-2 ambapo hatimaye wa Algeria hao wakafanikiwa kusonga mbele kwa ushindi wa mabao 5-3 ya magoli ya mikwaju ya penati.

Mlinzi Fares Abderahmane alifunga goli la penati zuri sana.
Kabla ya mchezo kocha msaidizi Kheireddine Madoui alikaririwa akisema 

"tutaonyesha miujiza ya kweli kwa kufuzu hatua ya makundi"

Majehi na kadi nyekundu na za njano zilipelekea Setif kuwakosa walinzi Mohamed Ziti na Farouk Belkaid (pichani), kiungo Mourad Delhoum na Amir Karaoui pamoja na washambuliaji Khaled Gourmi na Rachid Naji.

Mabingwa hao wa ligi ya Algerian maarufu kama Ligue 1 walilazimika kumtumia mlinda mlango Amar Saadoune kucheza ndani.

Kwingineko Saint George hii leo inasaka ushindi ili kuwa timu ya kwanza kutoka Ethiopia kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Hii leo walikuwa ugenini kucheza dhidi ya Enppi ya Misri wakiwa mbele na ushindi wa nyumbani wa mabao 2-0 magoli yaliyofungwa na kiungo Shimeles Bekele na mlinzi Abebaw Butako.

Saint George walikuwa na matumaini ya kufuzu katika michuano ya vilabu bingwa kabla ya matumaini yao kuondolewa na mabingwa wa soka nchini Misri mwezi mjini Cairo ambapo Zamalek walisonga mbele kwa faida ya bao la ugenini.

Enppi si pekee kutoka Misri ambao wanapigana kucheza hatua hiyo ya makundi kwani hata mabingwa wa zamani barani Afrika Ismaily nao wako katika vita ya kutaka kuidhoofisha CA Bizertin ya Tunisia ambao wako mbele kwa ushindi wa mchezo wa mkono wa kwanza wa mabao 3-0.
Bizertin inatokea katika mji wa Bizerte ambao uko kaskazini mwa nchini ya Tunisia.

Neymar: Ronaldo, Kaka & Marcelo walijaribu kunishawishi nijiunge na Madrid
 Neymar amesema kuwa Cristiano Ronaldo alijaribu kumshawishi ili ajiunge na Real Madrid.

Mbrazilo huyo alilazimika kuisikiliza zaidi familia yake kabla ya kuamua kujiunga na Barcelona na anasema kucheza timu moja na nyota kama Lionel Messi kwake ni heshima.

Neymar ametanabaisha kuwa Cristiano Ronaldo, Kaka na Marcelo walimshawishi sana ili ajiunge na Real Madrid msimu wa kiangazi kabla ya jaribio lao kushindikana.
Amenukuliwa akisema 

"Ronaldo, Kaka, Marcelo... Lots of people said I should sign for Real," Neymar told Marca. "But, in the end, I made a decision, which I discussed a lot with my family, and I'm very happy with the path I've chosen to play in Europe."

No comments:

Post a Comment