KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 24, 2013

Ghana na Nigeria wanatakiwa kuongeza nguvu Under-20

Ghana na Nigeria zimetakiwa kujitahidi na kujirekebisha endapo zitahitaji kufanya vema katika michuano ya kombe la dunia kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 fainali zake zikifanyika nchini Uturuki baada ya zote kuanza kwa vichapo.

Bingwa wa zamani Ghana alianza kwa kutereza mbele ya Ufaransa baada ya kukubali chapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Ufaransa ilhali Nigeria wakikubali mbele ya Ureno kwa kichapo cha mabao 3-2.

Kocha wa Ghana Sellas Tetteh, ambaye aliipa Ghana ubingwa mwaka 2009 amelalamikia sehemu yake ya ulinzi ya timu yake kuwa ilikuwa na tatizo.

Ufaransa waliapata bao la utangulizi kupitia kwa Geoffrey Kondogbia, kabla ya Yaya Sanogo kuongeza la pili muda mfupi baadaye.

Christophe Bahebeck aliandika bao la tatu kabla ya Yiadom Boakye kufunga bao la kufuatia majonzi kwa upande wa Black Satellites.

Kocha wa Nigeria Obuh, anasema anautaza mchezo ujao dhidi ya Cuba, baada ya kupokea kichapo cha kwanza kutoka kwa Ureno.

No comments:

Post a Comment