KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 24, 2013

Kocha wa Nigeria Keshi alalamikia umaliziaji mmbovu.


Kocha wa timu ya taifa ya soka ya Nigeria Stephen Keshi amesema kukosekana kwa umakini mbele ya goli la wapinzani wao Hispania lilikuwa tatizo kwao kiasi kupelekea kuondolewa kwao katika michuano ya kombe  la shirikisho nchini Brazil.

Mabingwa hao wa African wamemaliza wakiwa katika nafati ya tatu katika kundi lao baada ya kukubali kibano cha mabao 3-0 kutoka kwa Hispania mchezo uliopigwa usiku mwingi kwa saa za Afrika mashariki hiyo jana.

Katika michezo ya awali ya kundi hiyo Nigeria iliichapa Tahiti kwa mabao 6-1 kabla ya kupoteza kwa Uruguay kwa kufunga mabao 2-1.
Amenukuliwa keshi akisema tatizo tumeshindwa kutulia katika eneo la wapinzani, kitu kizuri ni kwamba tulikuwa tunatengeneza nafasi lakini hatukuwa tukimaliza vema.
"Hicho ni kitu ambacho tunapaswa kukifanyia kazi. Na ninaimani kukifanyia kazi haraka."

Nigeria ilitakiwa kushinda katika mchezo huo kusaka nafasi ya kutinga nusu fainali lakini sasa Hispania wamesonga mbele baada ya ushindi huo wa mabao yaliyofunga mwa Jordi Alba na Fernando Torres.

Matokeo hayo yanaifanya Hispania sasa kukutana na Italia Alhamisi katika mchezo wa nusu fainali ya pili huko Forteleza , ilhali Brazil ikijipanga kukutana na Uruguay huko Belo Horizonte siku ya Jumatano.

No comments:

Post a Comment