KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 3, 2013

HABARI ZA MICHEZO AFRIKA: Anzhi wataka Eto'o asicheze asiichezee Cameroon michezo ya kufuzu kombe la dunia NA St George imekuwa timu ya kwanza kutoka Ethiopian kutinga hatua ya makundi ya michunano ya kombe la shirikisho



Timu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi imeliandikia barua shirikisho la soka la Cameroon kutaka nchi hiyo isimtumie Samuel Eto'o katika michezo ijayo ya kampeni ya kuwania kufuzu kombe la dunia  mwaka 2014.

Mtaalamu wa mambo ya tiba za viungo wa klabu hiyo physiotherapist, Stijn Vandenbroucke, amesema mshambuliaji huyo yuko katika maumivu ya msuli aliyoyapata katika mchezo wa fainali ya Russian Cup.

Katika taarifa yao wamesema mshambuliaji huyo anatakiwa kupumzika kwa wiki chache.

Eto'o anatarajiwa kuwasili nchini Cameroon hii leo ili kwamba timu ya waangalizi wa afya ya Indomitable Lion nayo iweze kumfanyia uchunguzi.

Hata hivyo daktari wa timu ya Cameroon ndiye mwenye kauli ya mwisho ya kuamua kama Eto'o yuko fiti ama laa na kama ataweza kutumika katika mchezo wa june 9 dhidi ya Togo na mchezo mwingine dhidi ya DR Congo wiko moja baadaye.

Cameroon wanaongoza kungi I wakiwa na alama sita ikiwa mbele kwa alama moja dhidi ya Libya huku DR Congo ikiwa na lama nne na Togo ikiwa na alama moja.

St George imekuwa timu ya kwanza kutoka Ethiopian kutinga hatua ya makundi ya michunano ya kombe la shirikisho 
 St George imefanikiwa kuwa timu ya kwanza kutoka Ethiopian kufuzu kwa hatua ya makundi ya kombe la shirikisho barani Afrika licha ya hapo jana kupata kichapo kutoka kwa ENPPI ya Misri.

ENPPI ilishinda katika mchezo huo wa mkondo wa pili wa kwa bao 3-1 matokeo ambayo yalifanya matokeo ya jumla kusimama kuwa sare ya 3-3 lakini timu hiyo ya Ethiopian imefanikiwa kusonga mbele kwa faida ya sheria ya kupata bao la ugenini.

St George itaungana na Stade Malien ya Mali, Enugu Rangers ya Nigeria na Etoile du Sahel ya Tunisia katika kundi A la michuano hiyo.

Mabingwa wa Algerian Entente Setif, TP Mazembe ya DR Congo, FUS Rabat ya Morocco na CA Bizertin ya Tunisia zote zilipata ushindi katika michezo yao na sasa zinajumuika katika kundi B.

Mshambuliaji raia wa Ivory Coast Vincent Die Foneye alifunga bao la uongozi kwa wenyeji ENPPI baada ya dakika 25 za mchezo lakini Tesfaye Alebachew aliwapa wenyeji wakati mgumu kufuatia kusawazisha bao hilo dakika 12 baadaye.

Die Foneye kwa mara nyingine tena akaandika mabao yake mawili kwa kwa ENPPI katika dakika sita za mwisho na kundika “hat-trick” lakini haikufua dafu hivyo St George ikafuzu.

Stade Malien imeichapa Lydia LB Academic ya Burundi kwa bao 1-0 na kuandika ushindi wa jumla wa mabao 6-0.

Mabingwa mara mbili wa zamani CS Sfaxien wameondolewa mashindanoni kufuatia sare ya bila kufungana na Enugu Rangers ya Nigeria ambao wamepita kwa ushindi wa jumla wa bao 1-0.

FUS Rabat wenyewe wamefanikiwa kusonga mbele baada ya sare ya mabao 3-3 wa Rabat derby dhidi ya FAR Rabat hapo jana na hivyo kusonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-3.

Mchezaji wa zamani wa Hibernian Abdesselam Benjelloun aliwapa FUS bao la uongozi dakika tatu yan mchezo kabla ya Mustapha El Yousfi kusawazisha dakika 30 baadaye.

FAR wakaandika bao linguine la pili kupitia kwa Mustapha Allaoui kunako dakika ya 60 lakini mabao mawili ndani ya dakika tatu kupitia kwa Hicham Laroui na Benjelloun yakawapa uongozi FUS tena.
Hata hivyo dakika ya mwisho Youne
ss Hammal akaandika bao la kusawazisha kwa wanajeshi hao na kusonga mbele.

Kulikuwa na taarifa mbaya kwa waarabu wengine wa Misri Ismaili ambao wametolewa mashindano licha ya ushindi wa nyumbani wa bao 1-0 dhidi ya CA Bizertin Tunisia.

Watunisia hao wamesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabaoa 3-1 baada ya ushindi wa mchezo wa kwanza wa mabao 3-0.

TP Mazembe ya DR Congo, chini ya Patrice Carteron pia imesonga mbele  licha ya kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Liga Muculmana ya Mozambique.

No comments:

Post a Comment