KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 6, 2013

SOMA UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Benni McCarthy astaafu soka rasmi akiwa na umri wa miaka 35, Aston Villa kuwaacha Richard Dunne, Eric Lichaj na Andy Marshall, Bayern Munich yamuongezea mkataba Franck Ribery miaka miwili NA Arsene Wenger kuongezewa mkataba mwingine anasema mtendaji mkuu Ivan Gazidis.


Mfungaji bora wa muda wote wa Afrika kusini Benni McCarthy amestaafu soka rasmi akiwa naumri wa miaka 35.

McCarthy alikuwa akiichezea Orlando Pirates tangu mwaka 2011 alipoihama West Ham.

Amekaririwa akisema
"Soka lilikuwa zuri kwangu – limenipa wakati mzuri na kuniwezesha kuwa katika nafasi nzuri ya kuimarisha maisha yangu.
"kwa hilo najivunia."

Vilabu alivyopitia Benni McCarthy
    Orlando Pirates (S Africa)
    West Ham (England)
    Blackburn Rovers (England)
    FC Porto (Portugal)
    Celta Vigo (Spain)
    Ajax Amsterdam (Netherlands)
    Cape Town Spurs (S Africa)
    Seven Stars (S Africa).

Mzaliwa huyo wa Cape Town alikuwa akichezea ligi kuu ya Uholanzi, Hispania, Ureno na England, na kushinda taji la Eredivisie akiwa na Ajax na taji laligi ya Ureno mwaka 2004 akiwa na Porto ya Ureno wakati huo ikiwa chini ya Jose Mourinho.

Ameendelea kunukuliwa akisema
"Nimebarikiwa kufurahia kazi ya soka ambayo kutoka katika soka la mchangani vya viwanja vya Nyanga mpaka kushinda medali katika Uefa Champions League na kombe la dunia la vilabu – kiwango cha juu ambacho mchezaji anaweza kufanikisha katika soka la ngazi ya vilabu".

Amestaafu kama mfungaji bora wa kihistoria katika soka la kimataifa akifunga magoli 31 baada ya kushuka uwanjani mara 80.

Licha ya kuachwa katika timu ya taifa ya wakati timu ya taifa ilipokuwa wenyeji wa fainali ya kombe la dunia mwaka 2010, McCarthy aliifungia timu ya taifa ya nchi hiyo maarufu kama Bafana Bafana katika fainali za mwaka 1998 na 2002.

Alirejea Afrika kusini baada ya kuvitumikia vilabu vya Blackburn na West Ham nchini England kabla ya kujiunga na vijana wa kitongoji cha Soweto, Orlando Pirates mwaka 2011.
Ameshinda taji akiwa na Pirates mwaka 2012.

Aston Villa kuwaacha Richard Dunne, Eric Lichaj na Andy Marshall.
 Mlinzi wa kimataifa wa jamhuri ya Ireland Richard Dunne ni miongini mwa wachezaji watatu watakao achwa na Aston Villa.

Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 33 ameichezea Villa jumla ya michezo 111 tangu kujiunga nayo mwaka 2009 akitokea katika klabu ya Manchester City kwa uhamisho wa pauni milioni £5 mwezi September 2009.

Mlinzi wa pembeni Eric Lichaj mwenye umri wa miaka 24, na mlinda mlango Andy Marshall,mwenye umri wa miaka 38, nao pia wataondoka pamoja na Dunne, ilhali mlinzi Jean Makoun na mshambuliaji Simon Dawkins pia wakitarajiwa kuondoka.

Makoun mwenye umri wa miaka 30, anaelekea kujunga na Rennes ya Ufaransa kwa mkopo huku Dawkins, 25 akirejea Tottenham.

Dunne amemaliza msimu huu akiwa na matatizo ya msuli maumivu aliyoyapata katika mchezo aliocheza kwa dakika 25 dhidi ya Georgia mjini Dublin jumapili iliyopita.

Nyota wa kimataifa wa Cameroon Makoun, ambaye alijunga na Villa akitokea Lyon kwa ada ya pauni milioni £6 mwaka 2011, anarejea Ufaransa katika klabu ya Rennes alikochezea kwa mkopo.

Dawkins ambaye aliichezea Villa michezo minne baada ya kujunga nayo akitokea Spurs kwa mkopo mwezi January, ilhali mmarekani Lichaj akiichezea michezo 23 kikosi cha Paul Lambert msimu huu.

Bayern Munich yamuongezea mkataba Franck Ribery miaka miwili.
 Winga wa Bayern Munich Franck Ribery amesaini kuongeza mkataba wa miaka miwili na klabu yake hiyo ambao ni mabingwa wa vilabu Ulaya mkataba ambao utamuweka hapo mpaka 2017.

Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka , 30 aliisaidia Munich kuwa timu yan kwanza ya Ujerumani kushinda kwa pamoja mataji matatu ndani ya msimu mmoja yakiwemo mataji ya Bundesliga, European Cup na German Cup.

Mlinzi raia wa Belgiam Daniel Van Buyten mwenye umri wa miaka 35, naye anatarajiwa kusalia hapo kwa mwaka mmoja zaidi.

Bayern ndiyo timu ya kwanza  nchini Ujrumani kutwa mataji mengi yakiwemo ya ligi ya nyumbani na Ulaya ndani msimu mmoja.

Inakuwa ni timu ya saba kufanya hivyo barani Ulaya kama ilivyokuwa kwa Celtic mwaka 1967, Ajax mwaka 1972, PSV Eindhoven mwaka 1988, Manchester United mwaka 1999, Barcelona mwaka 2009 na Inter Milan mwaka 2010.

Arsene Wenger kuongezewa mkataba mwingine anasema mtendaji mkuu Ivan Gazidis

Mtendaji mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis anaamini kuwa meneja wao Arsene Wenger ataendelea kusalia kwa muhula mwingine.
Wenger mwenye umri wa miaka 63, anaanza msimu mpya ambao unakuwa ni wa mwisho ndani ya mkataba wake huku Arsenal wakitegemea kumpa mkataba mwingine.

Historia ya Wenger ndani ya Arsenal kwa kipindi chote
    2012-13: League - 4th; Champions League - last 16; FA Cup - 5th round; League Cup - 5th round
    2011-12: League - 3rd; Champions League - last 16; FA Cup - 5th round; League Cup - 5th round
    2010-11: League - 4th; Champions League - last 16; FA Cup - quarter-finalists; League Cup - finalists
    2009-10: League - 3rd: Champions League - quarter-finalists; FA Cup - 4th round; League Cup - 5th round
    2008-09: League - 4th; Champions League - semi-finalists; FA Cup - semi-finalists; League Cup - fifth round
    2007-08: League - 3rd; Champions League - quarter-finalists; FA Cup - 5th round; League Cup - semi-finalists
    2006-07: League - 4th; Champions League - last 16; FA Cup - 5th round; League Cup - runners-up
    2005-06: League - 4th; Champions League - runners-up; FA Cup - 4th round; League Cup - semi-finalists
    2004-05: League - 2nd; Champions League - last 16; FA Cup - winners; League Cup - 5th round

Amekaririwa Gazidis akisema
"Tumepata meneja safi. Tuna matumaini ya kuwa anataka kufanya kile anachokifanya kwa muda mrefu. Tuna amini anafanya hivyo.
"Kimya kimya na kwa wakati muafaka tutatangaza mpango wake mpya mara baada ya mambo kuwa mwenye nafasi"

Tottenham yamtaja Franco Baldini kuwa mkurugenzi wa ufundi.
 Tottenham inajipanga meneja wa zamani wa England assistant Franco Baldini kuwa mkurugenzi wake wa ufundi.
Mtaliano huyo mwenye umri wa miaka , 52, aliachia nafasi hiyo katika klabu ya Roma jumatano na atachukua nafasi katika klabu ya Spurs katika kazi ya kusimamia usajili na sera za uhamisho.

No comments:

Post a Comment