Kocha wa Ivory Coast Sabri Lamouchi jana alitangaza kikosi cha wachezaji 25 kabla ya kuikabili Senegal katika mchezo wa mkondo wa pili kusaka nafasi ya kucheza kombe la dunia (playoff game) uliopangwa kufanyika Novemba 16 katika mjini mkuu wa Morocco ambapo amemuacha kiungo wa Newcastle
Cheick Tiote baada ya kusimamisha.
Nyota wa FC Bale Geoffrey Serey Die pia anakabiliwa na adhabu ya kusimamishwa ambapo sasa wamejumuishwa mshambuliaji wa CSKA Moscow Seydou Doumbia na Mathis Bolly wa
Fortuna Dusseldorf.
Gervinho, ambaye hivi karibuni amerejea mazoezini katika klabu yake ya Roma baada ya kuwa majeruhi pia amejumuishwa katika orodha ya wachezaji wa kikosi hicho huku pia mkongwe Didier
Drogba na kiungo nyota Yaya Toure pamoja na Kolo Toure na Salomon
Kalou wakijumuishwa.
Tembo hao wa Ivory Coast waliawachapa simba wa milima ya Teranga 3-1 katika mchezo uliopigwa mwezi uliopita mjini Abidjan.
Kocha wa Senegal Alain Giresse amewaambia wanahabari kuwa wakati wa kutangaza kikosi kuwa ana matumaini ya kubadili matokeo ya mchezo uliopita na kupata tiketi ya kucheza kombe la dunia mwakani nchini Brazil.
Kikosi
Goalkeepers: Boubacar Barry (Lokeren, Belgium), Sylvain Gbohouo (Sewe Sport), Abdoul Karim Cisse (Africa Sports).
Defenders: Kolo Abib Toure (Liverpool, England), Benjamin
Angoua (Valenciennes, France), Serge Aurier (Toulouse, France), Souleman
Bamba (Trazbonspor, Turkey), Arthur Boka (Stuttgart, Germany), Viera
Diarrassouba (Caykur Rizespor, Turkey), Jean Daniel Akpa Akpo (Toulouse,
France), Didier Zokora (Trazbonspor, Turkey).
Midfielders: Jean-Jacques Gosso-Gosso (Glençlerbirligi SK,
Turkey), Ismael Diomande (Saint-Etienne, France), Max-Alain Gradel
(Saint-Etienne, France), Abdul Razack (Anzhi, Russia), Koffi Romaric
Ndri (Bastia, France), Yaya Toure (Manchester City, England).
Forwards: Lacina Traore (Anzhi, Russia), Wilfried Bony
(Swansae, England), Gervinho (AS Roma, Italy), Didier Drogba
(Galatasaray, Turkey), Salomon Kalou (Lille, France), Giovanni Sio (FC
Bale, Switzerland), Mathis Bolly (Dusseldorf, Germany), Seydou Doumbia
(CSKA Moscou, Russia).
No comments:
Post a Comment