Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binaadamu – Amnesty 
International limeshutumu “kiwango kikubwa cha unyanyasaji wa 
wafanyakazi wa ujenzi nchini Qatar, kwenye ripoti yake ya hivi punde.
Amnesty Internationa imeitaka Qatar kuitumia fursa ya kuandaa dimba la 
Kombe la Dunia mwaka wa 2022 kwa kuonyesha kuwa imejitolea kulinda haki 
za binaadamu. Ripoti ya Amnesty International inasema wafanyakazi wa 
kigeni wanaishi kama “wanyama“, neno ambalo shirika hilo limesema 
watafiti wake walimsikia mkurugenzi mmoja wa kampuni ya ujenzi 
akilitumia kuwaelezea wafanyakazi hao.
Salil Shetty ni Katibu Mkuu wa Amnesty International na anasema "Kitu
 kimoja ambacho tunaamini kinapaswa kutatuliwa haraka ni mfumo wa kutoa 
vibali vya kuondoka. Tunadhani hilo linastahili kushughulikiwa haraka. 
Matatizo ya ukiukaji wa haki za binaadamu kuhusiana na wafanyakazi wa 
kigeni nchini Qatar ni makubwa mno. Yamesambaa kote. Siyo matukio 
machache tu".
Serikali ya Qatar inapinga madai hayo kuwa inawanyanyasa wafanyakazi wa 
kigeni, ikisema itayaijumuisha ripoti hiyo katika uchunguzi ambao tayari
 ilianzisha. Nasser al-Khater kutoka kwa kamati ya Kombe la Dunia 2022 
nchini Qatar anasema nchi hiyo inajaribu kurekebisha sheria hizo….."ni 
nchi inayokuwa kwa kasi sana kwa idadi ya watu, na mojawapo ya nchi 
zinazokuwa kwa kasi kiuchumi ulimwenguni, hivyo ni wazi vitu haviwezi 
kuimarika kwa wakati mmoja."
Ripoti hiyo imetoa wito kwa Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA 
kulishinikiza taifa hilo la Guba kuimarisha mazingira ya wafanyakazi wa 
kigeni, wengi wao ambao wanatokea Kusini au Kusini mashariki mwa Asia.
Wafanyakazi hao wanalalamika kutolipwa mishahara yao, mazingira magumu 
na hatari ya kufanyia kazi, na viwango vya kushutusha vya malazi. Wengi 
wao wamekwama nchini Qatar wasiweze kuondoka. Wafanyakazi wengi pia 
wameripoti hali mbaya ya afya na viwango duni vya usalam
 

No comments:
Post a Comment