AC Milan wamerejea katika hali ya kuanza kushinda ikiwa chini ya kocha mpya Clarence Seedorf wakianza na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Spezia mchezo uliochezwa katika dimba la San Siro na kutinga katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Italian mchezo uliochezwa jana Jumatano.
Keisuke
Honda alikuwa na miongoni mwa wafungaji ukiwa ni mchezo wake wa kwanza akifunga goli la tatu kunako dakika ya 47 ya mchezo.
Kocha mkuu mpya wa Milan Clarence Seedorf (kushoto) akiwa na Rais Adriano Galliani
Bosi huyo mpya akitia saini jezi ya AC Milan baada ya kuwasili Linate Airport hapo jana
Nicola Ferrari aliwapa goli la kujifariji mashabiki takribani 7000 wa Spezia waliosafiri kuufuata mchezo huo katika dakika ya mwisho ya mchezo.
Kikosi cha Seedorf cha Milan kitakuwa wenyeji wa mchezo dhidi ya Udinese Jumatano ijayo
Usajili mpya wa Keisuke Honda akifunga kwa AC Milan dhidi ya Spezia
Napoli nayo iliichapa Atalanta 3-1 kuifuata Milan katika robo fainali.
Giuseppe De Luca aliwapa Atalanta bao la kuongoza la kushtukiza mchezo uliopigwa San Paolo kunako dakika ya 13 kabla ya Jose Callejon kusawazisha dakika moja baadaye kwa mpira mzuri wa kitaalamu 'volley' kutoka katika eneo la kona mbano.
Napoli wakaandika bao la pili kupitia kwa Lorenzo Insigne kunako dakika ya 72 ambalo lilipingwa wageni Atalanta na kupelekea kutolewa ya uwanja kwa mlinzi Mario Yepes.
No comments:
Post a Comment