Dream team: Van Persie, Ramos, Messi, Luiz, Aguero na Wilshere waunganishwa katika tangazo jipya la Pepsi. |
Wazo la kuwakusanya Lionel Messi, Robin van
Persie, Sergio Aguero, Vincent Kompany na Sergio Ramos katika timu moja ya mpira inawezekana linaweza lisiingie katika akili yako.
Lakini kampuni ya vinywaji baridi ya Pepsi imefanikiwa kuwakusanya wakali hao katika timu moja inayotambulika 'Pepsi's dream team for 2014' pamoja na wachezaji wengine 14 ikiwa ni sehemu yao ya kampeni yao ya sasa inaitwa 'Live for Now' ikiwaweka pamoja na kuongeza shauku mpya kwa walio wengi kuona 'beautiful game'.
Tangazo la hivi karibuni linaanzisha kampeni ijulikanayo '2014 Pepsi Football campaign' ambayo itawavutia mashabiki wa soka duniani kuwa wa sasa kupitia 'Live For Now' kwa kuwaonyesha nyota hao wakionekana kufurahia michezo huo tangu wakiwa wadogo.
Sura za wachezaji zitakuwa zikionekana katika kifungashio cha bati cha kinywaji hiyo wakati kampeni hiyo itakapokuwa ikiendelea.
Wachezaji walichaguliwa kuunda hiyo 'Dream team'.
Jack
Wilshere, David Luiz (Brazil), Juan Guillermo Cuadrado (Colombia),
Clint Dempsey (USA), Tarik Elyounoussi (Norway), Maynor Figueroa
(Honduras), Mario Gomez (Germany), Vincent Kompany (Belgium), Kemar
Lawrence (Jamaica), Victor Moses (Nigeria), Peter Osaze Odemwingie
(Nigeria), Oribe Peralta (Mexico), Andriy Pyatov (Ukraine), Mohamed
Salah (Egypt) and Gylfi Sigurdsson (Iceland).
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi amekaririwa akisema hivi
'Football ilikuwa ni shauku yangu tangu nikiwa mdogo na na ndio kitu ambacho naishi nacho kwasasa 'I live for now'.
'Najisikia faraja kuwa karibu na Pepsi tena na kuwakilisha 'brand' hiyo duniani nikiwa sehemu ya timu hii'
Mlinzi wa Chelsea na Brazil Luiz amenukuliwa akisema
'Nimefurahi sana kuwa sehemu ya timu ya Pepsi na najisikia faraja kuwa sehemu ya timu hiyo.
'Kwangu mimi, kucheza mpira wa miguu ni kama kufanya kitu kizuri kila sekunde na kuonyesha mapenzi kwenye mchezo wenyewe na mashabiki pia
Picha ya Messi wakati wa hafla ya Ballon d'Or akiwa na mpenzi wake Antonella Roccuzzo
No comments:
Post a Comment