KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 10, 2014

Bondia Ibrahim King ashinda mkanda wa WPBF nchini Zambia (source www.superdboxing.blogspot.com)

  Mkuu wa wilaya ya Kibondo Venance Mwamoto ameongoza mashabiki wa mchezo wa ngumi nchini katika mapokezi ya bondia Ibrahim Class Kingi CLASS Mawe aliyeshinda mkanda wa WPBF kwa kumchapa bondia wa Zambi Mwansa Kabinga katika uwanja wa Arthur Davis kwa KO ya roundi ya tisa na hivyo kumfanya kuwa mshindi mara mbili.
 Pichani juu ni bondia Shomari Milundi, kulia ni Promota aliyefanikisha safari hiyo Yaj Msangi, wadau Bilali Ngonyani na Rogers Masamu Picha na
www,superdboxingcoach.blogspot.com
Na Mwandishi Wetu
 
Bondia Mtanzania anaeshika boxrec namba moja nchini Ibrahimu Class 'King Class Mawe' amerudi na ubingwa wa WPBF  nchini akitokeza Zambia ambapo alifanikiwa kumpiga kwa K,O mbaya sana bondia Mwansa Kabinga wa Zambia mchezo uliochezwa
Arthur Davis Stadium, Kitwe, Zambia
 
akizungumzia safari yake ya kuelekea kunyakuwa ubingwa huo alisema amepata tabu sana wakiwa njiani ambapo wame ondoka alhamisi usiku sana na kufika jumamosi asubui nchini Kenya ambapo alizuiwa kutokana na kuwa na passiport ndogo hivyo akufanikiwa kwenda Zambia walivyofika kenya waka ongea na Balozi wa Tanzania wa Kenya akawasaidia ata hivyo ndege waliyokuwa wapande ilikuwa imesha ondoka zamani

baada ya hapo kuna pesa flani walitakiwa waongeze wakaongeza kiasi kwa kudunduliza wakasafili mpaka Zambia

hata hivyo bondia huyo ni mchezo wake wa kwanza kucheza nje ya nchi tangia ajiunge na ngumi za kulipwa na kufanikiwa kunyakuwa ubingwa huo ambao umemuweka katika ramani nyingine kabisa ya kimataifa zaidi


akitoa ahadi hiyo Mkuu huyo alisema watu wengi wanapenda mchezo wa ngumi hivyo kwa niaba ya serekali nitafanya jitiada nikupatie mchezo mmoja kwa ajili ya kutetea mkanda wako hata burundi ili uzidi kufahamika na kukuza kipaji chako

bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' ajawa nyuma kuwashukuru makocha wake ambao wamemwezesha kufika hapo ambapo ni Habibu Kinyogoli 'Masta' Kondo Nassoro, Sako  Mtulya na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye anamtafutia mapambano mbalimbali na humpa ushauli awapo ulingoni

No comments:

Post a Comment