KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, June 25, 2014

Brazil; Kocha wa Italia Cesare Prandeli ajiuzulu

Kocha wa Italia Cesare Prandeli amesema kuwa atajiuzulu baada ya mabingwa hao mara nne kubanduliwanje ya Kombe la Dunia nchini Brazil siku ya Jumanne.
Timu yake ilishindwa kufanya vyema katika mechi za makundi kwa mara ya pili mfululizo katika kombe la dunia.
Italia iliondolewa baada ya kushindwa kwa bao 1-0 na Uruguay katika mechi ya mwisho ya makundi.
“Nilichagua mfumo fulani wa ukufunzi na ndio sababu ninajiuzulu, kwa sababu haukufanya kazi,” alisema.
Aliongezea: “Kuna jambo ambalo limebadilika tangu nilipotia saini mkataba mpya. Sijui kwanini lakini yameshatukia ukishikwa shikamana .”
Kocha huyo alitia sahihi mkataba mpya mwezi Mei iliyopaswa kumpa fursa ya kuhudumu kama mkufunzi mkuu wa Azzurri hadi baada ya mashindano ya kuwania ubingwa wa bara Uropa Euro ya mwaka wa 2016.
Prandeli amechukua hatua hii baada ya kujiuzulu kwaa rais wa shirikisho la kandanda la Italia Giancarlo Abete.
“Nilizungumza na rais wa shirikisho na naibu wa rais Demetrio Albertini na nikawapa barua ya kujiuzulu kwangu. Ni jambo lisilobadilika,”
Licha ya kupoteza dhidi ya Costa Rica katika mechi yao ya pili, waitaliano walihitaji pointi moja tu ili kufuzu katika raundi ya muondoano kufuatia ushindi wao wa mechi ya kwanza dhidi ya Uingereza kwa mabao 2-1.
Lakini bao lake Diego Godin la dakika za mwisho baada ya Luiz Suarez kuepuka adhabu baada ya kile kinachodhaniwa kuwa alimng'ata beki wa Italia Girorgio Chiellini, iliwapa Uruguay ushindi na kuwabandua Italia .
Abete alisema: "Ningependa kutangaza kujiuzulu kwangu.
“Ninaamini kuwa katika mkutano ujao wa bodi wanaweza kumhimiza Cesare kusalia katika nafasi yake.”

No comments:

Post a Comment