KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 30, 2014

Mungu ibariki Afrika: Algeria bado iko vizuri kihistoria kuikamua Ujerumani

Algeria itavaana na Ujerumani hii leo katika mchezo mwingine wa hatua ya 16 bora ya michuano hiyo. 
Algeria iliyoingia kwa mara ya kwanza katika hatua hiyo ya 16 bora itakuwa inataka kuendeleza ubabe wake kwa Ujerumani ambayo ilikubali kichapo katika michezo miwili iliyowahi kukutana na mbweha hao wa jangwa.
Kocha wa Algeria Vahid Halilhodzic amesema ushindi mwaka 1982 utachangia kuwapa nguvu na ujasiri wachezaji wake katika mchezo wa leo huku Joechim Loew akisema kuwa mchezo huo hauna maana yoyote kwa wachezaji wa sasa kwakua wengi wao walikuwa hawajazaliwa.
Washindi katika michezo ya leo, watakutana katika hatua ya robo fainali ya kombe la dunia ambayo itaanza kuchezwa tarehe 4 ya mwezi huu.

No comments:

Post a Comment