KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, June 15, 2014

Tabarez: Sio kwamba Suarez hakuwa fiti katika mchezo wa kichapo cha Uruguay cha mabao 3-1 kutoka kwa Costa Rica

Luis Suarez akionyesha maumivu wakati muda ukiyoyoma wakiwa nyuma kwa mabao 3-1 dhidi ya Costa Rica
Luis Suarez alikuwa fiti kuweza kiasi kuwepo katika benchi lakini hakutumia katika mchezo dhidi ya Uruguay mchezo ambao uliamua matokeo ya kichapo cha mshituko kutoka kwa Costa Rica ukiwa ni mchezo wa ufunguzi wa kundi D wa fainali za kombe la dunia nchi Brazil.
Mshambuliaji huyo nyota wa Liverpool ni mmoja wa nyota wa dunia aliye katika kiwango safi hivi sasa hapo kabla alipatwa na jeraha la mguu ambalo lilihitaji upasuaji ambapo ungemuweka nje kwa takribani mwezi na hivyo kukosa fainali hizi.
Katika mchezo dhidi ya Costa Rica alikuwa katika benchi la wachezaji wa akiba akishuhudia kikosi chake cha Uruguay kikiadhibiwa kwa mabao 3-1.
Wakati Oscar Duarte akiandikisha bao la pili kwa Costa Rica, upande wa benchi alionekana Suarez alionekana wazi kuonyesha hisia za maumivu.

Devastated: Suarez looks on forlorn as they fall 3-1 to Costa Rica in their opening group D match
Suarez anashuhudia bao la tatu lililofanya matokeo ua 3-1 muda mfupi kabla ya filimbi ya mwisho ukiwa ni mchezo wa kundi D.

Warm up: Suarez shows he's ready to go on the sidelines
Star striker: The Liverpool marksman has had minimal time to recover from knee surgery but was named on the bench

Niingize mimi kocha: Suarez akiopasha misuli wakati mchezo ukiendelea.


Mabadiliko mawili yalifanywa dakika ya 60 akitoka Diego Forlan na Walter Gargano na kuingizwa Nicolas Lodeiro na Alvaro Gonzalez na kumuacha Suarez, mpiga mabao mwenye magoli mengi msimu uliopita katika ligi ya England 'Premier League' ama unaweza kumwita Golden boot winner akiachwa akisugua akiwa amevalia kishati cha mazoezi cha rangi ya kahawia ( pichani juu).
Uruguay ikafanya mabadiliko dakika ya 77 lakini Suarez akiwa kakalia benchi bila ya kutikisika. Abel Hernandez aliingia badala ya Cristian Rodriguez.
Kocha wa Uruguay Oscer Tabarez amekaririwa akisema Suarez alikuwa katika hali nzuri kucheza.
'Suarez alikuwa fiti kama asingekuwa fiti asingekuwepo katika benchi'.

Limbering up: Suarez went through the pre-match preparations with his team-mates
Suarez aliingia katika maandalizi ya mchezo wakati wa kupasha misuli moto.

No comments:

Post a Comment