KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 9, 2014

Usajili Ulaya: Alberto Moreno alekea Merseyside kukamilisha usajili

International: Liverpool wanamtaka Alberto Moreno (kulia). 

Liverpool wanatarajiwa kupiga hatua nyingine mbele hii katika kujaribu kumshawishi Alberto Moreno baada ya kukubali ada iliyotakiwa na Sevilla ya pauni milioni £16.2 usajili ambao unatazamwa kuwa unaweza kuongeza kiwango cha klabu hiyo.
Mlinzi huyo wa kushoto alitarajiwa hii leo kuelekea England na moja kwa moja kutinga Merseyside akiwa na baba yake na wakala wake Javier Moya.
Moreno alikuwepo katika sherehe za harusi ya nyota wa Liverpool Luis Alberto jumamosi iliyopita kwa mujibu wa gazeti la moja la nchini Hispania


Luis Alberto, ambaye aliondoka Sevilla kwenda Liverpool kiangzazi iliyopita kwa pauni milioni £7 amekuwa akijadili uwezekano wa mkopo kuelekea Malaga.
Kiunngo wa Liverpool Suso, ambaye hapo kabla alionekana kama mbadala wa Moreno, huenda sasa akaelekea nchini Ureno katika klabu ya Porto ambao tayari wameonyesha nia ya kumsajili.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 amesaliwa na mwaka mmoja wa mkataba wake na Porto wakiwa na nja ya kukamilisha mpango huo kwa haraka.
Liverpool pia wanapanga mazungumzo na Iago Aspas, ambaye wakala wake amesema kuwa anataka kusalia lakini huenda akauzwa endapo hajisikii kuendelea kusalia hapoa kwa kuwa mshambuliaji wa benchi.
Wanted: Suso may move to Porto with the Portuguese club expressing an interest in the midfielder
Wanted: Suso huenda akajiunga na Porto

Hughes asema na Barca juu ya kinda Traore (baada ya mpango wa Sidwell kukamilika)
Stoke wako katika ya kunyatia saini ya nyota anayeinukia wa Barcelona Adama Traore.
Meneja Mark Hughes amekamilisha usajili wa kiungo mzoefu Steve Sidwell mwenye umri wa miaka 31, lakini anatafuta uwezekano wa nguvu zaidi katika kikosi chake.
Akionekana kuvutiwa na mafanikio ya Gerard Deulofeu ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya Everton, Hughes amepiga hodi katika klabu yake ya zamani ya Barcelona kusaka uwezekano wa kupatokana kwa kinda huyo mwenye umri wa miaka 18 Traore, ambaye ni mmoja kati ya nyota kinda waliong'ara katika 'NextGen Series' na michuano ya UEFA Youth League.
Rising star: Stoke are exploring the possibility of signing Barcelona's Adama Traore (centre)
Stoke wanasaka huduma ya kinda wa Barcelona Adama Traore (katikati)

Traore alianza kucheza katika ligi ya Hispania  Liga Novemba akiwa na umri wa miaka 17, alipochukua nafasi ya Neymar katika mchezo wa ushindi wa uwanja wa nyumbani wa mabao 4–0 dhidi ya Granada. Siku tatu baadaye akaanza kucheza katika UEFA Champions League, akiingia kwa kuchukua nafasi ya Cesc Fabregas dakika ya 82 mchezo ambao Barca walichapwa 2-1 na Ajax.
Kinda huyu amezaliwa umbali mfupi kutoka Nou Camp na mama mmoja wa nyumbani huku baba yake akiwa ni mfanya kazi wa duka la kubadilisha wheel rims.
Adama anazichezea timu zote za vijana za Hispania za wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 19 lakini alibadilisha uhalali wake wa kimataifa kwa kujihalalisha na Mali.
Stoke ilimsajili Marc Muniesa kutoka Barcelona kiangazi iliyopita na inamatumaini ya kuendeleza uhusiano wake na klabu hiyo.
From Spain to England: Stoke defender Marc Muniesa (left) joined from Barcelona last year
From Spain to England: Stoke defender Marc Muniesa (left) joined from Barcelona last year

QPR wanasonga kwa Rio
Pendekezo lolote la usajili wa Rio Ferdinand kuelekea QPR linaweza kuonekana kama dhihaka au klabu hiyo ni kama inajaribu kuhoji hadhi ya mchezaji huyo.
Baadhi ndani ya klabu hiyo watataka wachezaji ambao hawaelekei ukiongoni katika uchezaji wao wa soka lakini wengine wanaona kuwa uzoefu na uwezo wa Ferdinand utakuwa msaada mkubwa kwa wachezaji wengine, lakini kuna wengine waonaona kuwa tayari klabu hiyo ina wazoefu wakutosha na kwamba pengine ni wakati wa kupata vijana zaidi.
QPR imeweka ofa mezani kwa mlinda mlango mwenye umri wa miaka 34 Rob Green ofa ya mkataba wa miaka mitatu na tayari wameweka mezani ofa za Clint Hill mwenye umri wa miaka 35, na Alejandro Faurlin mwenye umri wa miaka 27, wakati ambapo mlinda mlango Julio Cesar akirejea kutoka kwenye mkopo wa klabu ya Toronto lakini akitarajiwa kurejea nchini Brazil.
Searching: QPR may stall on a move for Rio Ferdinand who is looking for a club after leaving Manchester United
Searching: QPR huenda wakamsajili Rio Ferdinand baada ya Manchester United

Barcelona wanasema hapana kwa United wanaomchungulia Alba
Manchester United wamehusishwa na mlinzi wa kushoto wa Barcelona Jordi Alba wakati ambapo klabu yake ya nchini Hispania ikisema hapana mchezaji huyo hauzwi.
Barcelona wanafikiria kuongeza kibubu kwa kumuuza Cesc Fabregas, Pedro, Dani Alves and Alexis Sanchez lakini mchezaji Alba hayuko katika mapngo wa kuuzwa na kwamba ni sehemu ya mpango wa baadaye wa klabu hiyo.
United imekuwa ikiwasiliana na Barca kusaka uwezekano wa wachezaji wa Barca lakini Louis van Gaal hafikirii kuwapa kipaumbele.
Staying put: Barcelona have no desire to sell Spanish international Jordi Alba (right) despite interest from United
Staying put: Barcelona have no desire to sell Spanish international Jordi Alba (right) despite interest from United

Luke Shaw awaambia Southampton kuwa anadhamiria kujiunga na Manchester United mwishini mwa msimu na kwamba Mauricio Pochettino ataelekea Tottenham.
Southampton haiko katika mpango wa kutumia fedha nyingi kabla ya meneja mpya hajakamilisha makubaliano ya msingi.
Hivyo basi, Shaw na Liverpool wako katika mawindo ya Adam Lallana na imeelezwa wazi kuwa wapia watakuwepo msimu ujao na kwamba sio St Mary.
Manchester-bound? Luke Shaw told Southampton he wanted to join United at the end of last season
Luke Shaw awaambia Southampton kuwa anataka kujiunga United mwisho wa msimu.


Sunderland yamtupia jicho Jakupovic kulinda lango.
Sunderland wanataka kumsajili mlinda mlango wa Hull City Eldin Jakupovic.
Meneja Gus Poyet ana orodha ndefu ya magolikipa ambapo Jakupovic akipewa nafasi kubwa ambapo atakwenda kuwa namba mbili wa Allan McGregor ambaye amekuwa akijiimarisha katika nafasi hiyo.

Thumbs up: Hull City goalkeeper Eldin Jakupovic impressed on loan at Leyton Orient last season
Thumbs up: Hull City goalkeeper Eldin Jakupovic impressed on loan at Leyton Orient last season

Set to move: Hill City striker Matty Fryatt (left) will speak to Nottingham Forest on Monday
Set to move: Hill City striker Matty Fryatt (left) will speak to Nottingham Forest on Monday
Napoli kuamua juu ya Pennant Samaras
Napoli huenda ikapiga chini wazo la kuwasajili wachezaji wawili huru Jermaine Pennant na nyota wa Celtic Georgios Samaras.
Kwasasa wanaonyesha kumtaka Sandro wa Tottenham huku suala la ada ya uhamisho likisali kuwa ni kikwazo. Tottenham pia kwa mara nyingine wanaonekana kumtaka Mirko Vucinic wa Juventus ingawaje pia anayakiwa na Valencia.
On duty: Greece striker Georgios Samaras arrives at the team hotel in Brazil ahead of the World Cup
On duty: Greece striker Georgios Samaras arrives at the team hotel in Brazil ahead of the World Cup


Tottenham na Everton zimeonyesha nia ya kumsajili kiungo wa Granada Yacine Brahimi ambaye atakuwepo katika kikosi cha timu ya taifa ya Algeria katika fainali za kombe la dunia.
Wasaka vipaji wa Everton pia walikuwepo katika mchezo kupasha misuli moto kabla ya kombe la dunia jumamosi baina ya Croatia na Australia.

 Mshambuliaji wa Hull Nikica Jelavic alifunga goli moja pekee la ushindi la Croatia. Alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Arsenal mpiga mabao wa Chelsea Mario Mandzukic ambaye ameripotiwa kutaka kuihama Bayern Munich kiangazi.

No comments:

Post a Comment