KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 10, 2014

Wallece Karia na Sunday Kayuni watoa neno kwa makocha nchini Tanzania

Makamu wa Rais wa TFF Wallace Karia
Makamu wa Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF, Wallace Karia hii leo amezindua kozi ya Leseni B inayotambuliwa na Shirikisho la barani Afrika CAF.

Wallace Karia amezindua kozi hiyo inayoshirikisha makocha zaidi ya 20 wenye Leseni C kutoka Tanzania Bara pamoja na Zanzibar chini ya wakufunzi wanaotambuliwa na shirikisho la soka barani Afrika CAF
Sunday Kayuni pamoja na Salum Madadi ambae ni mkurugenzi wa Ufundi wa TFF.

Karia amewataka makocha wanaoshiriki katika kosi hiyo kuwa wasikivu kwa ajili ya kupata elimu ya soka ambayo itakuwa kichocheo kikubwa katika maendeleo ya mchezo huo hapa nchini.
 
Sanday Kayuni
Nae mkufunzi mkuu katika kozi hiyo Sunday Kayuni Amesema anaamini mafunzo yatakayotolewa katika kizo hiyo inayofanyika jijini Dar es salaam itakuwa ni motisha kwa makocha washiriki kwenda kuendeleza elimu katika vilabu vyao ili kutimila malengo yanayokusudiwa na shirikisho la soka nchini TFF.
Kwa upande wa washiriki ambao waliwakilishwa na kocha kituo cha kulea na kuendeleza vipaji kwa vijana cha wakati ujao Wane Nelson Mkisi amesema hawana budi kuyafanyia kazi wanayojifunza katika kozi hiyo, hivyo amemuahidi makamu wa raisi wa TFF Wales Karina kutarajia mabadiliko siku za usoni.

No comments:

Post a Comment