KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 16, 2014

YAPOKEA MALALAMIKO KUHUSU MKUTANO WA YANGA

Mwenyekiti wa Yanga Yusufu Manji
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea malalamiko kuhusu uamuzi uliofanywa na Mkutano Mkuu wa Yanga uliofanyika Juni Mosi mwaka huu ambao ulimuongezea muda wa mwaka mmoja mwenyekiti wa klabu hiyo Yusufu Manji kinyume na katiba ya klabu hiyo.
 TFF imesema inasubiri muhtasari wa mkutano huo kutoka kwa uongozi wa Yanga ili tuweze kutoa mwongozo kama ikibidi.
Mwenyekiti wa klabu ya Yanga SC Yusuf Manji aliwaongoza wanachama hai wapatao 1,560 kupitisha kipengele kipya alichokiita ni kwa ajili ya maslahi na faida ya Wana Yanga kwani bila kufanya hivyo timu isingeweza kuruhusiwa kushiriki Ligi Kuu msimu ujao.
Aidha katika mkutano huo Manji aliwatoa hofu wanachama kwa kuwaambia kuwa usajili unaendelea kufanyika na nafasi zilizobakia ni nne tu hivyo pindi utakapokamilika basi wataweka wazi kila kitu.

No comments:

Post a Comment