KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 8, 2014

Klabu bingwa nchini Uingereza Man City, imekamilisha dili la usajili wa mlinda mlango kutoka nchini Argentina, Willy Caballero.

Manchester City, imethibitisha kumsajili golikipa Willy Caballero
Klabu bingwa nchini Uingereza Man City, imekamilisha dili la usajili wa mlinda mlango kutoka nchini Argentina, Willy Caballero akitokea kwenye klabu ya Malaga ya nchini Hispania kwa ada ya uhamisho wa paund million 6.5.

Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 32, amekwenda Etihad Stadium kwa urahisi, kufuatia mahusiano mazuri yaliopo kati ya viongozi wa Malaga pamoja na meneja wa Man city, Mannuel Pellgrini.

Dhumuni kubwa la Pellegrini la kumsajili Caballero ni kutaka kumpa changamoto mlinda mlango Joe Hart, ambaye ni chaguo lake la kwanza kuhakikisha anatunza uwezo wake katika kipindi chote cha msimu ujao, la sivyo huenda akaipoteza nafasi hiyo.

Dakika kadhaa baada ya kukamilisha usajili wa kujiunga na Man City, Caballero amezungumza na kituo cha televisheni cha klabu hiyo na kuelezea furaha yake ambapo amesema ni faraja iliyoje kwake kujiunga na klabu kubwa tena yenye sifa mjini Manchester na kwingineko.

“Ujio wangu Man City natambua ni mtihani kwangu pamoja na Joe Hart, itanilazimu kucheza kwa kujituma wakati wote kwa ajili ya kutimiza malengo yangu na ya klabu pia.” Amesema Willy Caballero

“Nafahamu Joe Hart ni mlinda mlango mzuri, tena mwenye viwango vya hali ya juu, lakini ujio wangu haumaanishi kama nimekuja hapa nishindane naye, ila nina uhakika kila mmoja atapewa nafasi kutokana na uwezo wake wa kuisaidia klabu ya Man city yenye lengo la kutaka kutetea ubingwa wa Uingereza msimu ujao.” Amesisitiza Caballero.

Kusidio lingine la kusajiliwa kwa Willy Caballero huko Etihad Stadium ni kuziba nafasi iliyoachwa wazi na mlinda mlango kutoka nchini Romania Costel Fane Pantilimon, ambaye ametimkia kwenye klabu ya Sunderland kufuatia mkataba wake kumalizika.

No comments:

Post a Comment