KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 25, 2014

KOCHA MAXIMO WA YANGA ANASEMA ANASUBIRI BARUA RASMI YA USHIRIKI WA KOMBE LA KAGAME.

Maximo akitoa vitu kwa mshambuliaji Jerson Tegete
 KAGAME CUP RWANDA
Kocha mkuu wa Dar es salaam Young Africans Marcio Maximo amesema klabu yake inasubiri barua maalum kutoka baraza la vyama vya soka ukanda wa Afrika mashariki na kati CECAFA na kujua nini cha kufanya.
Maximo ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika muda mfupi baada ya mazoezi uwanja wa shule ya sekondari ya Loyola iliyoko Mabibo jijini Dar es Salaam.
Maximo ambaye anaonekana kukiamini mno kikosi chake kwa sasa amesema anasubiri kauli ya CECAFA kupitia kwa viongozi wake na kwamba kikosi chake kipo vizuri.
Maximo amesema taarifa ambazo amezipata mpaka mapema hii leo asubuhi ni kwamba viongozi wa baraza la vyama vya soka afrika mashariki na kati CECAFA bado hawajaiarifu klabu ya Dar es salaam Young Africans juu ya ushiriki wa michuano ya mwaka huu.
Amesema endapo barua ya kuarifiwa kwa Dar es salaam Young Africans kutoka CECAFA itawasili hata tesho asubuhi na akapewa ruhusana kuondoka na kikosi chake kwenda Kigali Rwanda, hatosita kufanya hivyo kutokana na kuhitaji michezo ya ushindani kwa ajili ya kujiwinda na msimu mpya wa ligi.

Katika hatua nyingine
Kwa upande wa maandalizi ya kikosi, Maximo amesema kikosi chake kinaendelea vyema na mazoezi ya kila siku kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Loyola jijini Dar es salaam.
Amesema mbali na mazoezi pia amekuwa akiwahusia wachezaji wake suyala la kujituma na kuweka mbele uzalendo wa kuitumikia Dar es salaam young Africans ambayo inahitaji kutoka hapa ilipo na kwenda mbele zaidi.
Amesema kwake yeye mchezaji mwenye nafasi ni yule anayejituma na kujitoa kwa timu na si mchezaji mbinafsi.

No comments:

Post a Comment