KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, July 23, 2014

MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA YAFUNGULIWA RASMI HII LEO

Michuano ya jumuia ya Madola kwa mwaka 2014, imefunguliwa rasmi hii leo jijini Glasgow nchini Scotland huku mataifa 71 yakitarajiwa kushindana katika michezo 17 tofauti, ambayo itaanza kutimua vumbi lake kesho.

Tayari waziri mkuu wa nchini Scotland, Alex Salmond ameshathibitisha kukamilika kwa maandalizi ya michuano hiyo ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa michezo duniani kote, huku kila nchi ikiamini wawakilishi wao wataibuka na medali ima za dhahabu, shaba ama fedha.

Salmond amewataka wachezaji kutoka kila kona ya dunia kujihisi wapo nyumbani na washiriki michuano hiyo kwa amani ambayo itafikia tamati August 3.
Hata hivyo kiongozi huyo amewasihi wanamichezo watakaoshiriki michuano ya Jumuia ya Madola kwa mwaka huu huko mjini Glasgow, kujiepusha na kadhia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu michezoni, ili kuepuka balaa ambalo huenda likawaharibia maisha yao ya baadae katika nyanja ya kimichezo.

Amesema vipo vinywaji vya kawaida ambavyo vinatumika na vinaruhusiwa kwa wanamichezo kuvitumia wakati wote, lakini wasithubutu kwenda nje ya maadili kwa kunywa vinywaji ama dawa zenye chembe chembe za kuongeza nguvu.

Waziri mkuu wa nchini Scotland, Alex Salmond.

Michezo itakayoshindaniwa katika michuano ya jumuia ya madola kwa mwaka huu ni Kurusha tufe, riadha, mbio za baiskeli, masumbwi, kuogelea, kuchupa kwenye maji, Judo, mpira wa pete, Rugby, mpira wa meza, kunyanyua vitu vizito, mieleka, Squash, Sarakasi, mpira wa magongo, kulenga shabaha pamoja na Badminton.

No comments:

Post a Comment