KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 8, 2014

STARS YAINGIA KAMBINI TUKUYU KUFUATA BARIDI

Mart Noij kocha wa Stars
Wakati Taifa Stars inaingia kambini Tukuyu mkoani Mbeya kesho (Julai 9 mwaka huu), kocha Martinus Ignatius 'Mart Nooij' amesema kambi ya wiki mbili nchini Botswana imekisaidia kikosi chake kujiandaa kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.

Mart Nooij amesema kikosi chake kipo vizuri kuelekea katika mchezo wa kwanza wa hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco dhidi ya timu ya taifa ya Msumbiji.

Nooij ametangaza uhakika huo hii leo mbele ya waandishi wa habari ambapo amesema utayari wa kikosi chake kuikabili Msumbiji umekuja kufutia maandalizi mazuri waliyofanya mjini Gaborone nchini Botswana kwa muda wa majuma mawili.

Amesema kesho watakuwa wakielekea mjini Tukuyu mkoani Mbeya kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya mchezo huo ambao umepangwa kufanyika Julai 20 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Akizungumzia safari yake ya nchini Msumbiji ambayo aliifanya kabla ya kuelekea Botswana nooij amesema hakwenda mjini Maputo kwa kusudio la kuwachunguza wapinzani wake The Mambas balia likwenda kukamilisha shughuli zake binafsi za kimaisha.

Hata hivyo kocha huyo kutoka nchini Uholanzi amekataa kata kata kutoa ahadi kwa mashabiki wa soka nchini kuelekea katika mchezo huo dhidi ya Msumbiji kwa kusema sio desturi yake kuahidi matokeo ili hali mchezo husika ukiwa bado haujachezwa.

Kwa msisitizo zaidi Mart Nooij akatumia mfano wa mchezo wa tennis kwa kusema mashabiki wa mschezo huo huwa hawaamini kama washiriki wanaweza kushinda michezo yote, halia mbayo anaichukulia na kwake kama kocha wa Taifa Stars.

Lakini pamoja na kusisitiza itikadi hiyo, Nooij amesema bado ataendelea kutumia mfumo wa uchezaji kama alivyofanya wakati wa mchezo dhidi ya Zimbabwe ambapo kikosi chake kilionekana kutumia nafasi pale ilipo patikana.

Kitaalamu amesema kambi ya Tukuyu kama ilivyokuwa ya Botswana itawasaidia kwa mechi dhidi ya Msumbiji.
 Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka kwa ndege kwenda Mbeya ikiwa na kikosi cha wachezaji 25, na itarejea jijini Dar es Salaam siku tatu kabla ya mechi hiyo.
 Wachezaji walioko kwenye msafara huo ni Aggrey Morris, Aishi Manula, Amri Kiemba, Benedictor Tinoko, Deogratius Munishi, Edward Charles, Emmanuel Namwando, Erasto Nyoni, Haruni Chanongo, Himid Mao, John Bocco na Jonas Mkude.
Wengine ni Joram Mgeveke, Kelvin Friday, Kelvin Yondani, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa, Mwagane Yeya, Nadir Haroub, Oscar Joshua, Pato Ngonyani, Ramadhan Singano, Said Juma, Said Moradi, Shomari Kapombe na Simon Msuva.
 Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Afrika (AFCON) dhidi ya Msumbiji itafanyika Julai 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment