KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 15, 2014

CRISTIANO RONALDO AFIKISHA WAFUASI MILIONI 100 WA MTANDAO WA FACEBOOK

Nyota shupavu wa kandanda Cristiano Ronaldo ameweka historia kama mwanaspoti wa kwanza duniani kupata wafuasi milioni 100 kupitia ukurusa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa Face Book.
Ronaldo amefikia idadi hiyo jana Jumanne na kuingia kumbukumbu kama binadamu wa pili katika historia kufikia idadi hiyo nyuma ya mwanamziki mashuhuri, Rihanna.
Wanamuziki wenye sifa ulimwenguni, Eminem (milioni 96) na mwanadada Shakira (milioni 90) ndio wanafunga nne bora kwenye orodha hiyo ya watu wenye ‘wapendwa’ au kwa Kimombo ‘likes’ nyingi zaidi kwenye kurasa zao za Face Book.
Ronaldo ambaye aliifungia taifa lake Ureno goli la ushindi Jumanne usiku kwenye mechi ya kufuzu Kombe la Euro 2016 dhidi ya Denmark amekuwa mhusika mkuu kwenye mtandao huo tangu kufungua ukurasa wake 2009.
Nyota huyo wa miamba wa Uhispania Real Madrid ametumia ukurasa huo kupatia mashabiki wake fursa ya maisha ya ukwasi wanaspoti mashuhuri huishi.
Matangazo yake na picha anazoweka kwenye mtandao huo haswa akijivinjari na sabuni yake ya roho, Irina Shayk likizoni zimetia fora sana na kuvutia wengi kupenda ukurasa wake.
“Ni heshima kubwa kwangu kufikia ‘wapendwa’ milioni 100 wa Facebook. Ni jambo la kushangaza kupanda ngazi hii ya utukufu na kuwasiliana na mashabiki wangu kote duniani. Wao ndio hunipa motisha na nawashukuru wote,” Ronaldo alisema kwenye taarifa.
Nyota mwenzake na asimu mkubwa wa Barcelona, Lionel Messi anamfuata miongoni mwa wanaspoti na ‘wapenzi’ milioni 74.

No comments:

Post a Comment