KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, March 13, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA MICHEZO: Olivier Groud anasema goli la mapema muhimu dhidi ya Munich. Mlinda mlango wa Chelsea Thibaut Courtois anogewa na Atletoco Madrid. Bosi wa Liverpool anasema kiangazi ni kusaka Ubora na wingi. Mikel Arteta ataka Arsenal kuwekeza majira ya kiangazi kama wanataka mataji. Franz Beckenbauer anasema Pep Guardiola anachangamoto kubwa ya mafanikio Bayern Munich na Gennaro Gattuso kustaafu rasmi kiangazi. .

Mshambuliaji wa washika bunduki wa London Arsenal ya nchini England Olivier Giroud, amesema kuwa goli la mapema katika mchezo wao dhidi ya Bayern Munich ni muhimu, ili kufanikisha mpango wao kupata matokeo mazuri ya kusonga mbele kwa hatua ya robo fainali ya michuano ya vilabu bingwa Ulaya usiku wa leo.

Washika bunduki hao wamesafiri kuelekea Allianz Arena nchini Ujerumani wakiwa nyuma kimatokeo, ambapo wanalazimika kubadilisha matokeo ya kuwa nyuma kwa 3-1 dhidi ya Bayern Munich,  ambao tangu mwezi Oktoba hawajapoteza mchezo.

Giroud, bila kujali nafasi ya Arsenal ilivyo kwasasa, amesema kuwa ameangalia aina ya uchezaji wa Bayern Munich na anadhani Munich maarufu kama ‘Bavarians' wanafungika.

Giroud ambaye hajafunga katika michezo sita ambayo Arsenal imekuwa ikicheza ugenini, anaamini anaweza kufanya hivyo dhidi Bayern hii leo kufuatia kauli ya nyota wa Munich Thomas Mueller kusisitiza kuwa hawatacheza mchezo wa kujilinda kwa kuwa wako mbele kimatokeo.

@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@



Mlinda mlango wa Chelsea Thibaut Courtois anogewa na Atletoco Madrid.

Thibaut Courtois amethibitha juu ya matamanio yake ya kuendelea kusalia na Atletico Madrid msimu ujao badala ya kurejea katika klabu yake aliyokulia ya Chelsea ya England.

Raia huyo wa  Belgiam katika kampeni ya misimu miwili iliyopita, alikuwa na klabu hiyo yenye maskani yake katika mji mkuu wa Hispania wa Madrid, klabu ambayo ilifanikiwa kushinda mataji mawili ya Europa League na UEFA Super Cup ikiwa ni pamoja na kucheza fainali ya Copa del Rey.

 Courtois mpaka sasa bado hajaichezea klabu yake iliyomkuza ya Chelsea ambayo alimsaini kutoka katika klabu ya Genk inayoshiriki ligi ndogo inayotambulika kama Jupiler Pro League mwaka  2011.

Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 21 ametanabaisha kuwa hana haraka ya kurejea Stamford Bridge na kuwa kama mlinda mlango namba mbili Petr Cech.


Aidha Courtois, ambaye ameweka rekodi ya kucheza dakika 820 bila kuruhusu goli kabla ya mchezo wa Jumapili ambapo walipoteza dhidi ya Real Sociadad kwa bao 1-0, amesema anajua kuwa hatma yake baadaye iko nje ya maamuzi yake

Amenukuliwa akisema

"Nina furaha, nafurahia maisha hapa na wenzangu katika kikosi. Si maamuzi yangu , Chelsea na Atletico wnapaswa kuongea".


@@@@@@@@@@@@@@@

Bosi wa Liverpool anasema kiangazi ni kusaka Ubora na wingi.

Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amesisitiza kuwa klabu yake itakuwa ikisaka ubora na sio ujazo wakati atakapo kuwa katika kazi kuboresha kikosi chake wakati wa soko la wachezaji la kipindi cha kiangazi.

Kwasasa wekundu hao wako katika mwendo mzuri wa ushindi baada ya kushinda michezo yao mitatu ya mwisho ya ligi kuu ya England ‘Premier League’ huku Manchester United na Tottenham wakifanya vema kwa kukusanya alama zaidi tangu kuanza kwa mwezi Desemba.

Rodgers anaamini kuwa kuongezeka kwa Daniel Sturridge na Phillippe Coutinho mwezi Januari kumeongeza nguvu na uhai ndani ya kikosi na kusisitiza kuwa ongezeko la wachezaji wenye ubora katika kipindi cha majira ya kiangazi kutarejesha changamoto mpya ya kiushindani zaidi katika nafasi za juu. 

"Tunasaka ubora sasa na si uwingi"

"Tunaona matokeo ya ubora wa Coutinho na Sturridge, hicho ndicho tunachokitafuta. Endapo tutawaleta wengine watatu au wanne wa kiwango hicho, tukichanganya na hao tulionao tutakuwa na kikosi cha nguvu ambacho kitaweza kushindana"

Rodgers alivurugwa na jaribio la kumchukua Clint Dempsey kushindikana msimu wa kiangazi uliopita, timu ya utafutaji wa  wa wachezaji kitasaidia kuleta wachezaji wa kweli wakati huu.

Anaamini kuwa Liverpool iko sawa katika kila idara na itaendelea kuongeza vipaji.
 @@@@@@@@@@@@@@@

Mikel Arteta ataka Arsenal  kuwekeza majira ya kiangazi kama wanataka mataji.
Kiungo nyota wa klabu ya Arsenal, Mikel Arteta anaamini kuwa kunatakiwa kufanyika uwekezaji wa kutosha katika kipindi cha majira ya kiangazi kama klabu hiyo inataka kutafuta mataji tena msimu ujao.
Baada ya timu hiyo kung’olewa katika Kombe la Ligi na Bradford City na lile la FA na Blackburn Rovers timu hiyo imekosa matumaini ya kunyakuwa taji lolote msimu huu ikiwa imepita miaka nane toka walipofanya hivyo mwaka 2005.
Arteta anafikiri kuwa pengo kati ya vinara wa Ligi Kuu nchini Uingereza Manchester United na timu hiyo ni kubwa na kuonya kuwa bodi lazima igundue kuwa wanaporomoka kutoka katika ushindani kabla hawajachelewa.
Nyota huyo aliendelea kusema kuwa klabu hiyo ina msingi mzuri kuliko klabu yoyote ambayo amewahi kucheza na pia mfumo mzuri, wachezaji wazuri na fedha za kutosha ambazo wanaweza kufanya chochote hivyo haoni sababu kwanini klabu hiyo inasuasua badala ya kutumia nafasi hiyo kuwa kileleni.
Wachezaji wengi nyota huvutiwa kwenda katika klabu ambayo watapata uhakika wa kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hivyo hivyo Arteta anaamini kama Arsenal itakuwa ikishindwa kushika nafasi nne za juu ni wazi inaweza kuporomoka kiushindani kama ilivyokuwa hapo awali.
@@@@@@@@@@

Franz Beckenbauer anasema Pep Guardiola anachangamoto kubwa ya mafanikio Bayern Munich.

Nguli wa soka wa zamani nchini Ujerumani, Franz Beckenbauer amedai kuwa meneja mtarajiwa wa klabu ya Bayern Munich Pep Guardiola atakuwa chini ya shinikizo kubwa kufikia mafanikio yaliyowekwa msimu huu na meneja wa sasa Jupp Heynckes.
Kocha huyo wa zamani wa Barcelona anatarajiwa kuchukua mikoba ya kuinoa Bayern Julai mosi mwaka huu lakini Heynckes ambaye ataondoka mwishoni mwa msimu ametengeneza pengo kubwa katika mbio za ubingwa wa Bundesliga kitu ambacho kinamuogopesha Beckernbauer.
Bayern kwasasa inaongoza Bundesliga kwa tofauti ya alama 20 baada ya kupambana kutoka nyuma mara mbili na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Fortuna Duesseldorf Jumamosi iliyopita.
Klabu hiyo kama ikishinda mechi tatu za ligi zinazofuata itakuwa tayari wametawazwa mabingwa wapya wa Bundesliga hiyo ikiwa ni mara ya 23 kushinda taji hilo.
Nguli huyo anadai kuwa kila mtu anafikiri mambo yanaweza kubadilika kwa klabu hiyo wakati Guardiola atapoanza kufundisha hivyo kama timu itachukua ubingwa kwa tofauti ndogo ya alama kuliko msimu huu watu wanaweza kukosa imani naye.
Maneno ya nguli huyo yaliungwa mkono pia na rais wa Bayern Uli Hoeness ambaye amesema anafikiri timu hiyo itakuwa bingwa wa ligi msimu huu hivyo shinikizo kwa Guardiola na klabu litakuwa kubwa.
@@@@@@@@@@@

Gennaro Gattuso kustaafu rasmi kiangazi.
Kiungo nyota wa zamani wa kimataifa wa Italia na klabu ya AC Milan, Gennaro Gattuso amesema anatarajia kustaafu rasmi kucheza soka katika kipindi cha majira ya kiangazi ili aweze kuhamishia nguvu zake kwenye ukocha.
Gattuso mwenye umri wa miaka 35 ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya FC Sion ya Switzerland amedai anadhani wakati wa kutundika daruga umefika baada ya kucheza kwa kipindi cha miaka 18.
Nguli huyo amesema mara baada ya kuacha kucheza soka anataka kujitolea kwa nguvu zake zote katika kazi yake mpya ya ukocha ili aweze kupata mafanikio kama ilivyokuwa wakati akicheza soka.
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa amepata uzoefu wa kutosha wakati akiwa mchezaji chini ya makocha Marcello Lippi na Carlo Ancelotti kwani walikuwa walimu wazuri kwake wakati akiwa Milan.
FC Sion ambayo kwasasa inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Switzerland maarufu kama Swiss Super League wanatarajia kusafiri kwenda Geneve Jumapili kupambana na timu ya Young Boys.
@@@@@@@@@@

No comments:

Post a Comment