KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, October 4, 2013

Tottenham yang'aa kwenye Uropa

Michuano ya ligi ya Uropa ilienndelea hapo jana, katika kundi K Tottenham ya uingereza iliivuta chini Anzhi Makhachkala ya urusi huko Moscow kwa mabao mawili kwa bila.
 Katika Mechi nyingine Swansea ya uingereza iliishinda St Gallen ya uswizi kwa bao moja kwa bila na kuchukua uongozi katika kundi A
Wakati huo huo kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson ameendelea kusisitiza kuwa lije jua ama mvua, kipa wake nambari moja ni Joe Hart.
 Mlinda lango huyo wa Man City alilaumiwa na wakosoaji wengi katika mechi ya Jumatano dhidi ya Bayern Munich wakisema kuwa uzembe wake ulichangia kwa kiasi kikubwa kuifanya timu yao kuwa taabani mikononi mwa Beyern iliyoicharaza mabao matatu kwa moja katika michuano ya klabu bingwa ulaya.
Wakati Mashabiki wa Man City wakiuma vidole vyao kuhusu utendaji kazi wa kipa wao, wapo baadhi ya Mashabiki wa Man U nao wanaosema kocha David Moyes ameshindwa kazi lakini wamekumbushwa na mtangulizi wake Sir Alex Fergeson kuwa Moyes anatosha.
 Ikiwa hilo ni kweli au la itajulikana, viwanjani ila kwa sasa Man U inashikilia nafasi ya kumi na mbili katika msimamo wa ligii ya Uingereza jambo ambao limewaacha wengi kujiuliza hatima ya Man U wanaotetea taji hilo.

No comments:

Post a Comment