KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, December 5, 2012

USIKU WA ULAYA MANCHESTER CITY WAAGA KWA AIBU ILHALI ARSENAL NAO WAKISHIKISHWA ADABU NA OLYMPIAKOS.HABARI NA MATUKIO KATIKA PICHA .


Olympiakos iliyotokea nyuma imefanikiwa kuichapa Arsenal mjini Piraeus, na kuwafanya washika mitutu hao kumaliza katika nafasi ya pili katika kundi B nyuma ya Schalke.

Tomas Rosicky alianza kufunga bao la uongozi kwa Arsenal kabla ya bao la kipindi cha pili la Giannis Maniatis lililokuwa la kusawazisha na baadaye Kostas Mitroglou kuandika bao la pili na la ushindi kwa wagiriki.

Kocha wa Schalke Leonardo Jardim aliwatumia wachezaji wake ambao ni wafungaji wakubwa katika ligi ya Ugiriki  Rafik Djebbour na Djamel Abdoun sehemu ya kiungo.

Akiwa ni mwenye matumaini ya kufuzu, Wenger alikifanyia mabadiliko kikosi chake kilichopoteza dhidi ya Swansea mabao 2-0 mwishoni mwa juma akimrejesha Rosicky kiungoni pamoja na kinda wa miaka 20 Jernande Meade akicheza dakika zote za mchezo.

MANCHESTER CITY 0 VS DOTMUND 1
Manchester City imemaliza kampeni ya michuano ya ligi ya mabingwa ulaya kwa kichapo kingine cha bao 1-0 toka  Borussia Dortmund.
Bao la kipindi cha pili la Julian Schieber kunako dakika ya 57 lilitosha kuwaondosha katika harakati za kusonga mbele na michuano hiyo huku wajerumani wakifurahia mchezo ambapo walitengeneza nafasi nyingi karibu sehemu kubwa ya mchezo.
Matokeo hayo yana maanisha kuwa kikosi cha Roberto Mancini kimemaliza michezo yake ya kundi D kikiwa mkiani bila ushindi hata mmoja na Dortmund wakifanikiwa kusonga mbele katika hatua ya mtoano ya michuano hiyo.
 
  •   MATOKEO MENGINE
  • Din Zagreb     1 - 1     Dynamo Kiev FT
  • Malaga       2 - 2     Anderlecht FT
  • Montpellier      1 - 1           Schalke 04 FT
  • Paris SG      2 - 1         FC Porto FT
  • Real Madrid   4 - 1               Ajax FT
AC Milan      0 - 1   Zenit St P'sbg

No comments:

Post a Comment