Shrikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha
mchezaji wa zamani wa timu za Coastal Union, TPC na Taifa Stars, Behewa
Ali Sembwana (72) kilichotokea jana usiku (Machi 31 mwaka huu) mkoani
Tanga.
Msiba
huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti
Sembwana akiwa mchezaji, alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali
alizochezea, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Sembwana
aliyekuwa akicheza wingi ya kulia alidumu katika Taifa Stars kwa miaka
kumi, kama ilivyokuwa kwa kombaini ya Mkoa wa Tanga (Tanga Stars)
aliyoiwakilisha katika michuano ya Kombe la Taifa (Taifa Cup).
TFF
inatoa pole kwa familia ya marehemu Sembwana, Chama cha Mpira wa Miguu
Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na
subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko
yanatarajiwa kufanyika leo (Aprili 1 mwaka huu) kijijini kwake Lusanga,
Wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana
mahali pema peponi. Amina
No comments:
Post a Comment