KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, July 3, 2013

Nigeria yatolewa kombe la dunia. Liverpool wamsajili Kolo Toure, Swansea City yakamilisha usajili wa Jonjo Shelvey kwa pauni milioni £5 .BAADA YA KUJIUNGA NA REAL MADRID ISCO ANA MATUMAINI YA KUPATA NAFASI YA KUCHEZA KOMBE LA DUNIA, Vito Mannone asajiliwa na Sunderland akitokea Arsenal.

 Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Ivory Cost Kolo Toure kutoka Manchester City.
Toure mwenye miaka 32 amesajiliwa na Liverpool kwa mkataba wa miaka miwili baada ya mkataba na Man City wanaomilikiwa na kampuni ya Etihad kumalizika.
Ameichezea City jumla ya michezo 102 baada ya kusajiliwa akitokea Arsenal mwaka 2009 kwa pound milioni 14, lakini alicheza mechi 18 pekee msimu uliopita na kujikuta akiachwa kwenye kikosi cha wachezaji wa Man City walioshiriki michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.
Kolo Toure anaenda Merseyside baada ya aliyekuwa nahodha msaidizi wa klabu hiyo Jamie Carragher kutundika daruga huku hatma ya beki kitasa wa timu hiyo rais wa Slovakia Martin Skrtel ikiwa haijulikani.
Ameuambia mtandao wa klabu hiyo hatua hiyo ina maana kubwa kwake, na amejiunga na moja klabu bora nchini England.
"Nilipoondoka City ilikuwa ni muhimu kwangu kubaki England kwa kuwa ni ligi bora na kuja Liverpool ni hatua kubwa kwangu."
"Nimeichagua Liverpool kutokana na historia yake na hamasa ya wachezaji wanavyoitumikia timu yao." Alisema Toure.
Katika misimu saba aliyocheza Arsenal, Toure alishinda Kombe la FA mara mbili na alikuwa miongoni mwa kikosi cha Arsenal ambacho kiliandika historia ya kucheza ligi ya 2003-04 bila kufungwa hata mechi moja.
Mwaka 2011 alikosa kombe la FA walilochukua Man City kwa kufungiwa miezi sita kutokana kushindwa kufanya vipimo vya madawa ya kuongeza nguvu michezoni.
Toure ni mchezaji wa nne kusajiliwa na Liverpool baada ya klabu hiyo kumsajili, Luis Alberto na Lago Aspas pamoja na mlinda mlango Simon Mignolet aliyesajiliwa akitokea Sunderland.

Swansea City yakamilisha usajili wa Jonjo Shelvey kwa pauni milioni £5 .
Swansea City imekamilisha usajili wa kiungo Jonjo Shelvey kutoka klabu ya Liverpool kwa uhamisho wa pauni milioni £5.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 21 ambaye aliichezea England kwa mara ya kwanza dhidi ya San Marino oktoba 2012, amesaini mkataba wa miaka minne.
Crystal Palace iliyokuwa pia katika vita ya kumnasa kiungo huyo sasa wamesalimu amri.
Shelvey ambeye ameichezea Liverpool kwa michezo 17tangu ajiunge nayo akitokea Charlton Athletic mwaka 2010, anakuwa mchezaji wa sita wa kudumu wa Swansea kusajiliwa msimu huu wa kiangazi.
Ametuma salamu kwa mashabiki wa Liverpool kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter akisema "Nitalikumbuka sana jiji na klabu pia asanteni sana, ni wakati wa kufungua ukurasa mpya wa maisha yangu kule Wales. Asanteni."

BAADA YA KUJIUNGA NA REAL MADRID ISCO ANA MATUMAINI YA KUPATA NAFASI YA KUCHEZA KOMBE LA DUNIA
Isco wa Real Madrid anamatumaini kuwa kuhama kwake kutamuongezea nafasi ya kucheza katika kombe la dunia akiwa na kikosi cha timu ya Hispania
Amejiunga na klabu hiyo akitokea Malaga kwa ada ailiyoripotiwa ya pauni £23 na kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na meneja mpya Carlo Ancelotti.
Isco amesaini mkataba wa miaka mitano baada ya kufanikiwa katika vipimo vyake afya.

    Born: Benalmadena, Spain, on 21 April 1992
    Clubs: Valencia B, Valencia, Malaga, Real Madrid
    International: Spain - one appearance

Isco amekabidhiwa jezi nambari 23 namba ambayo ilikuwa ikitumiwa na David Beckham wakati akiitumikia  Bernabeu.
Amenukuliwa akisema
"Sote tunamjua Beckham ni mchezaji mkubwa na aliitumia kwa miaka 10, lakini nimechagua namba hii kwasababu ni siku ya kuzaliwa kaka yangu ".

Vito Mannone asajiliwa na Sunderland akitokea 
Arsenal
Sunderland imemsajili mlinda mlango wa Arsenal Vito Mannone kwa ada ambayo haikuwekwa wazi.
Mannone mwenye umri wa miaka 25, alijunga na Atalanta mwaka 2005, na kuvichezea vilabu vya Barnsley na Hull City kwa mkopo.
Mchezo wake wa mwisho uliokamilisha utumishi wake wa michezo 26 ulikuwa ni baina ya Arsenal na Fulaham mchezo uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3 mwezi November 2012.
Kuwasili kwake kwa mkataba wa miaka miwili kunafuatia kuondoka hivi karibuni kwa mlinda mlango nambari moja Simon Mignolet kuelekea Liverpool kwa pauni milioni £9.
Mannone aliaanza kuichezea Arsenal miaka minne baada ya kujiunga nayo akitokea Barnsley katika msimu wa mwaka 2006-07.

Nigeria yatolewa kombe la dunia.

Matumaini ya Nigeria yan kuchukua kwa mara ya kwanza taji la kombe la dunia kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 yamemalizwa na Uruguay katika hatua ya mtoano ya timu 16 za mwisho katika michuano ambayo ambayo inafanyika nchini Uturuki.
Nigeria maarufu kama Flying Eagles ilipunguzwa wachezaji wake na kusaliwa na wachezaji 10 uwanjani kabla ya mapunziko imepoteza mchezo huo kwa kuachapwa mabao 2-1.
Nicolas Lopez alifunga magoli yote mawili ya Uruguay likiwemo moja la penati ilhali Olarenwaju Kayode alifanikiwa kufunga goli kwa upande wa Nigeria.
Ghana inakuwa ndiyo timu ya mwisho kutoka katika bara la Afrika kusalia katika michuano hiyo na hii leo wanakabiliwa na mchezo wa hatua hatua hiyo dhidi ya Ureno.
Mali na mabingwa wa African Misri zimeshindwa kuvuka na kuingia katika hatua hiyo inayofanyika nchini Uturuki.

No comments:

Post a Comment